< Psalmorum 59 >

1 Psalmus, in finem, ne corrumpas, David in tituli inscriptionem, quando misit Saul, et custodivit domum eius, ut eum interficeret. Eripe me de inimicis meis Deus meus: et ab insurgentibus in me libera me.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Wakati Sauli alipotuma wapelelezi nyumbani mwa Daudi ili wamuue. Ee Mungu, uniokoe na adui zangu, unilinde kutokana na hao wanaoinuka dhidi yangu.
2 Eripe me de operantibus iniquitatem: et de viris sanguinum salva me.
Uniponye na watu watendao mabaya, uniokoe kutokana na wamwagao damu.
3 Quia ecce ceperunt animam meam: irruerunt in me fortes.
Tazama wanavyonivizia! Watu wakali wananifanyia hila, ingawa Ee Bwana, mimi sijakosea wala kutenda dhambi.
4 Neque iniquitas mea, neque peccatum meum Domine: sine iniquitate cucurri, et direxi.
Sijatenda kosa; hata hivyo wako tayari kunishambulia. Inuka unisaidie, uone hali yangu mbaya!
5 Exurge in occursum meum, et vide: et tu Domine Deus virtutum, Deus Israel, Intende ad visitandas omnes gentes: non miserearis omnibus, qui operantur iniquitatem.
Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli! Zinduka uyaadhibu mataifa yote, usionyeshe huruma kwa wasaliti.
6 Convertentur ad vesperam: et famem patientur ut canes, et circuibunt civitatem.
Hurudi wakati wa jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
7 Ecce loquentur in ore suo, et gladius in labiis eorum: quoniam quis audivit?
Tazama yale wanayotema kutoka vinywa vyao, hutema upanga kutoka midomo yao, nao husema, “Ni nani atakayetusikia?”
8 Et tu Domine deridebis eos: ad nihilum deduces omnes gentes.
Lakini wewe, Bwana, uwacheke; unayadharau mataifa hayo yote.
9 Fortitudinem meam ad te custodiam, quia Deus susceptor meus es:
Ee nguvu yangu, ninakutazama wewe, wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu,
10 Deus meus misericordia eius praeveniet me.
Mungu wangu unipendaye. Mungu atanitangulia, naye atanifanya niwachekelee wale wanaonisingizia.
11 Deus ostendit mihi super inimicos meos, ne occidas eos: nequando obliviscantur populi mei. Disperge illos in virtute tua: et depone eos protector meus Domine:
Lakini usiwaue, Ee Bwana, ngao yetu, au sivyo watu wangu watasahau. Katika uwezo wako wafanye watangetange na uwashushe chini.
12 Delictum oris eorum, sermonem labiorum ipsorum: et comprehendantur in superbia sua. Et de execratione et mendacio annunciabuntur
Kwa ajili ya dhambi za vinywa vyao, kwa ajili ya maneno ya midomo yao, waache wanaswe katika kiburi chao. Kwa ajili ya laana na uongo wanaotamka,
13 in consummatione: in ira consummationis, et non erunt. Et scient quia Deus dominabitur Iacob: et finium terrae.
wateketeze katika ghadhabu, wateketeze hadi wasiwepo tena. Ndipo itakapofahamika katika miisho ya dunia kwamba Mungu anatawala juu ya Yakobo.
14 Convertentur ad vesperam, et famem patientur ut canes: et circuibunt civitatem.
Hurudi jioni, wakibweka kama mbwa, wakiuzurura mji.
15 Ipsi dispergentur ad manducandum: si vero non fuerint saturati, et murmurabunt.
Wanatangatanga wakitafuta chakula, wasipotosheka hubweka kama mbwa.
16 Ego autem cantabo fortitudinem tuam: et exaltabo mane misericordiam tuam. Quia factus es susceptor meus, et refugium meum, in die tribulationis meae.
Lakini mimi nitaziimba nguvu zako, asubuhi nitaimba juu ya upendo wako; kwa maana wewe ndiwe ngome yangu na kimbilio langu wakati wa shida.
17 Adiutor meus tibi psallam, quia Deus susceptor meus es: Deus meus misericordia mea.
Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.

< Psalmorum 59 >