< Psalmorum 50 >

1 Psalmus Asaph. Deus deorum Dominus locutus est: et vocavit terram, A solis ortu usque ad occasum:
Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
2 ex Sion species decoris eius.
Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
3 Deus manifeste veniet: Deus noster et non silebit. Ignis in conspectu eius exardescet: et in circuitu eius tempestas valida.
Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 Advocavit caelum desursum: et terram discernere populum suum.
Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 Congregate illi sanctos eius: qui ordinant testamentum eius super sacrificia.
“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 Et annunciabunt caeli iustitiam eius: quoniam Deus iudex est.
Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
7 Audi populus meus, et loquar Israel, et testificabor tibi: Deus Deus tuus ego sum.
“Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
8 Non in sacrificiis tuis arguam te: holocausta autem tua in conspectu meo sunt semper.
Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
9 Non accipiam de domo tua vitulos: neque de gregibus tuis hircos.
Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
10 Quoniam meae sunt omnes ferae silvarum, iumenta in montibus et boves.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
11 Cognovi omnia volatilia caeli: et pulchritudo agri mecum est.
Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
12 Si esuriero, non dicam tibi: meus est enim orbis terrae, et plenitudo eius.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
13 Numquid manducabo carnes taurorum? aut sanguinem hircorum potabo?
Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
14 Immola Deo sacrificium laudis: et redde Altissimo vota tua.
Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
15 Et invoca me in die tribulationis: eruam te, et honorificabis me.
na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
16 Peccatori autem dixit Deus: Quare tu enarras iustitias meas, et assumis testamentum meum per os tuum?
Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
17 Tu vero odisti disciplinam: et proiecisti sermones meos retrorsum:
Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Si videbas furem, currebas cum eo: et cum adulteris portionem tuam ponebas.
Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
19 Os tuum abundavit malitia: et lingua tua concinnabat dolos.
Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
20 Sedens adversus fratrem tuum loquebaris, et adversus filium matris tuae ponebas scandalum:
Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
21 haec fecisti, et tacui. Existimasti inique quod ero tui similis: arguam te, et statuam contra faciem tuam.
Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
22 Intelligite haec qui obliviscimini Deum: nequando rapiat, et non sit qui eripiat.
“Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
23 Sacrificium laudis honorificabit me: et illic iter, quo ostendam illi salutare Dei.
Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

< Psalmorum 50 >