< Psalmorum 46 >

1 Psalmus, in finem, pro filiis Core pro occultis. Deus noster refugium, et virtus: adiutor in tribulationibus, quae invenerunt nos nimis.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Propterea non timebimus dum turbabitur terra: et transferentur montes in cor maris.
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 Sonuerunt, et turbatae sunt aquae eorum: conturbati sunt montes in fortitudine eius.
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 Fluminis impetus laetificat civitatem Dei: sanctificavit tabernaculum suum Altissimus.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 Deus, in medio eius, non commovebitur: adiuvabit eam Deus mane diluculo.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Conturbatae sunt gentes, et inclinata sunt regna: dedit vocem suam, mota est terra.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 Dominus virtutum nobiscum: susceptor noster Deus Iacob.
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Venite, et videte opera Domini, quae posuit prodigia super terram:
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 auferens bella usque ad finem terrae. Arcum conteret, et confringet arma: et scuta comburet igni:
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
10 Vacate, et videte quoniam ego sum Deus: exaltabor in gentibus, et exaltabor in terra.
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
11 Dominus virtutum nobiscum: susceptor noster Deus Iacob.
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

< Psalmorum 46 >