< Psalmorum 41 >

1 Psalmus David, in finem. Beatus vir qui intelligit super egenum, et pauperem: in die mala liberabit eum Dominus.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 Dominus conservet eum, et vivificet eum, et beatum faciat eum in terra: et non tradat eum in animam inimicorum eius.
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 Dominus opem ferat illi super lectum doloris eius: universum stratum eius versasti in infirmitate eius.
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
4 Ego dixi: Domine miserere mei: sana animam meam, quia peccavi tibi.
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5 Inimici mei dixerunt mala mihi: Quando morietur, et peribit nomen eius?
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6 Et si ingrediebatur ut videret, vana loquebatur, cor eius congregavit iniquitatem sibi. Egrediebatur foras, et loquebatur
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7 in idipsum. Adversum me susurrabant omnes inimici mei: adversum me cogitabant mala mihi.
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8 Verbum iniquum constituerunt adversum me: Numquid qui dormit non adiiciet ut resurgat?
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9 Etenim homo pacis meae, in quo speravi: qui edebat panes meos, magnificavit super me supplantationem.
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
10 Tu autem Domine miserere mei, et resuscita me: et retribuam eis.
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11 In hoc cognovi quoniam voluisti me: quoniam non gaudebit inimicus meus super me.
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12 Me autem propter innocentiam suscepisti: et confirmasti me in conspectu tuo in aeternum.
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13 Benedictus Dominus Deus Israel a saeculo, et usque in saeculum: fiat, fiat.
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.

< Psalmorum 41 >