< Psalmorum 38 >

1 Psalmus David, in recordationem sabbati. Domine ne in furore tuo arguas me, neque in ira tua corripias me.
Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Quoniam sagittae tuae infixae sunt mihi: et confirmasti super me manum tuam.
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
3 Non est sanitas in carne mea a facie irae tuae: non est pax ossibus meis a facie peccatorum meorum.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
4 Quoniam iniquitates meae supergressae sunt caput meum: et sicut onus grave gravatae sunt super me.
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
5 Putruerunt et corruptae sunt cicatrices meae, a facie insipientiae meae.
Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Miser factus sum, et curvatus sum usque in finem: tota die contristatus ingrediebar.
Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7 Quoniam lumbi mei impleti sunt illusionibus: et non est sanitas in carne mea.
Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
8 Afflictus sum, et humiliatus sum nimis: rugiebam a gemitu cordis mei.
Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
9 Domine, ante te omne desiderium meum: et gemitus meus a te non est absconditus.
Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku yako wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako.
10 Cor meum conturbatum est, dereliquit me virtus mea: et lumen oculorum meorum, et ipsum non est mecum.
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniishia; hata macho yangu yametiwa giza.
11 Amici mei et proximi mei adversum me appropinquaverunt, et steterunt. Et qui iuxta me erant, de longe steterunt: et vim faciebant qui quaerebant animam meam.
Rafiki na wenzangu wananikwepa kwa sababu ya majeraha yangu; majirani zangu wanakaa mbali nami.
12 Et qui inquirebant mala mihi, locuti sunt vanitates: et dolos tota die meditabantur.
Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
13 Ego autem tamquam surdus non audiebam: et sicut mutus non aperiens os suum.
Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
14 Et factus sum sicut homo non audiens: et non habens in ore suo redargutiones.
nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
15 Quoniam in te Domine speravi: tu exaudies me Domine Deus meus.
Ee Bwana, ninakungojea wewe, Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.
16 Quia dixi: Nequando supergaudeant mihi inimici mei: et dum commoventur pedes mei, super me magna locuti sunt.
Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie, wala wasijitukuze juu yangu mguu wangu unapoteleza.”
17 Quoniam ego in flagella paratus sum: et dolor meus in conspectu meo semper.
Kwa maana ninakaribia kuanguka, na maumivu yangu yananiandama siku zote.
18 Quoniam iniquitatem meam annunciabo: et cogitabo pro peccato meo.
Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
19 Inimici autem mei vivunt, et confirmati sunt super me: et multiplicati sunt qui oderunt me inique.
Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari, wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.
20 Qui retribuunt mala pro bonis, detrahebant mihi: quoniam sequebar bonitatem.
Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.
21 Ne derelinquas me Domine Deus meus: ne discesseris a me.
Ee Bwana, usiniache, usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.
22 Intende in adiutorium meum, Domine Deus salutis meae.
Ee Bwana Mwokozi wangu, uje upesi kunisaidia.

< Psalmorum 38 >