< Psalmorum 34 >

1 Psalmus David, cum immutavit vultum suum coram Achimelech, et dimisit eum et abiit. Benedicam Dominum in omni tempore: semper laus eius in ore meo.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 In Domino laudabitur anima mea: audiant mansueti, et laetentur.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Magnificate Dominum mecum: et exaltemus nomen eius in idipsum.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 Exquisivi Dominum, et exaudivit me: et ex omnibus tribulationibus meis eripuit me.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Accedite ad eum, et illuminamini: et facies vestrae non confundentur.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Iste pauper clamavit, et Dominus exaudivit eum: et de omnibus tribulationibus eius salvavit eum.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 Immittet angelus Domini in circuitu timentium eum: et eripiet eos.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Gustate, et videte quoniam suavis est Dominus: beatus vir, qui sperat in eo.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Timete Dominum omnes sancti eius: quoniam non est inopia timentibus eum.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Divites eguerunt et esurierunt: inquirentes autem Dominum non minuentur omni bono.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Venite filii, audite me: timorem Domini docebo vos.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Quis est homo qui vult vitam: diligit dies videre bonos?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Prohibe linguam tuam a malo: et labia tua ne loquantur dolum.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Diverte a malo, et fac bonum: inquire pacem, et persequere eam.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Oculi Domini super iustos: et aures eius in preces eorum.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Vultus autem Domini super facientes mala: ut perdat de terra memoriam eorum.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Clamaverunt iusti, et Dominus exaudivit eos: et ex omnibus tribulationibus eorum liberavit eos.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Iuxta est Dominus iis, qui tribulato sunt corde: et humiles spiritu salvabit.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Multae tribulationes iustorum: et de omnibus his liberabit eos Dominus.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Custodit Dominus omnia ossa eorum: unum ex his non conteretur.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 Mors peccatorum pessima: et qui oderunt iustum delinquent.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Redimet Dominus animas servorum suorum: et non delinquent omnes qui sperant in eo.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psalmorum 34 >