< Psalmorum 33 >

1 Psalmus David. Exultate iusti in Domino: rectos decet collaudatio.
Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
2 Confitemini Domino in cithara: in psalterio decem chordarum psallite illi.
Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
3 Cantate ei canticum novum: bene psallite ei in vociferatione.
Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
4 Quia rectum est verbum Domini, et omnia opera eius in fide.
Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
5 Diligit misericordiam et iudicium: misericordia Domini plena est terra.
Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
6 Verbo Domini caeli firmati sunt: et spiritu oris eius omnis virtus eorum.
Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
7 Congregans sicut in utre aquas maris: ponens in thesauris abyssos.
Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
8 Timeat Dominum omnis terra: ab eo autem commoveantur omnes inhabitantes orbem.
Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
9 Quoniam ipse dixit, et facta sunt: ipse mandavit, et creata sunt.
Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
10 Dominus dissipat consilia gentium: reprobat autem cogitationes populorum, et reprobat consilia principum.
Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
11 Consilium autem Domini in aeternum manet: cogitationes cordis eius in generatione et generationem.
Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
12 Beata gens, cuius est Dominus, Deus eius: populus, quem elegit in hereditatem sibi.
Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
13 De caelo respexit Dominus: vidit omnes filios hominum.
Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
14 De praeparato habitaculo suo respexit super omnes, qui habitant terram.
kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
15 Qui finxit sigillatim corda eorum: qui intelligit omnia opera eorum.
yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
16 Non salvatur rex per multam virtutem: et gigas non salvabitur in multitudine virtutis suae.
Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
17 Fallax equus ad salutem: in abundantia autem virtutis suae non salvabitur.
Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
18 Ecce oculi Domini super metuentes eum: et in eis, qui sperant super misericordia eius.
Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
19 Ut eruat a morte animas eorum: et alat eos in fame.
ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
20 Anima nostra sustinet Dominum: quoniam adiutor et protector noster est.
Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
21 Quia in eo laetabitur cor nostrum: et in nomine sancto eius speravimus.
Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
22 Fiat misericordia tua Domine super nos: quemadmodum speravimus in te.
Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.

< Psalmorum 33 >