< Psalmorum 149 >
1 Alleluia. Cantate Domino canticum novum: laus eius in ecclesia sanctorum.
Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
2 Laetetur Israel in eo, qui fecit eum: et filiae Sion exultent in rege suo.
Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
3 Laudent nomen eius in choro: in tympano, et psalterio psallant ei:
Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
4 Quia beneplacitum est Domino in populo suo: et exaltavit mansuetos in salutem.
Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
5 Exultabunt sancti in gloria: laetabuntur in cubilibus suis.
Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
6 Exultationes Dei in gutture eorum: et gladii ancipites in manibus eorum:
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
7 Ad faciendam vindictam in nationibus: increpationes in populis.
kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
8 Ad alligandos reges eorum in compedibus: et nobiles eorum in manicis ferreis.
Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
9 Ut faciant in eis iudicium conscriptum: gloria haec est omnibus sanctis eius. Alleluia.
Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.