< Psalmorum 149 >

1 Alleluia. Cantate Domino canticum novum: laus eius in ecclesia sanctorum.
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 Laetetur Israel in eo, qui fecit eum: et filiae Sion exultent in rege suo.
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 Laudent nomen eius in choro: in tympano, et psalterio psallant ei:
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Quia beneplacitum est Domino in populo suo: et exaltavit mansuetos in salutem.
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 Exultabunt sancti in gloria: laetabuntur in cubilibus suis.
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 Exultationes Dei in gutture eorum: et gladii ancipites in manibus eorum:
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 Ad faciendam vindictam in nationibus: increpationes in populis.
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 Ad alligandos reges eorum in compedibus: et nobiles eorum in manicis ferreis.
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 Ut faciant in eis iudicium conscriptum: gloria haec est omnibus sanctis eius. Alleluia.
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< Psalmorum 149 >