< Psalmorum 141 >

1 Psalmus David. Domine clamavi ad te, exaudi me: intende voci meae, cum clamavero ad te.
Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
2 Dirigatur oratio mea sicut incensum in conspectu tuo: elevatio manuum mearum sacrificium vespertinum.
Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
3 Pone Domine custodiam ori meo: et ostium circumstantiae labiis meis.
Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
4 Non declines cor meum in verba malitiae, ad excusandas excusationes in peccatis. Cum hominibus operantibus iniquitatem: et non communicabo cum electis eorum.
Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
5 Corripiet me iustus in misericordia, et increpabit me: oleum autem peccatoris non impinguet caput meum. Quoniam adhuc et oratio mea in beneplacitis eorum:
Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
6 absorpti sunt iuncti petrae iudices eorum. Audient verba mea quoniam potuerunt:
Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
7 sicut crassitudo terrae erupta est super terram. Dissipata sunt ossa nostra secus infernum: (Sheol h7585)
Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
8 quia ad te Domine, Domine oculi mei: in te speravi, non auferas animam meam.
Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
9 Custodi me a laqueo, quem statuerunt mihi: et a scandalis operantium iniquitatem.
Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
10 Cadent in retiaculo eius peccatores: singulariter sum ego donec transeam.
Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.

< Psalmorum 141 >