< Psalmorum 135 >

1 Alleluia. Laudate nomen Domini, laudate servi Dominum:
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Qui statis in domo Domini, in atriis domus Dei nostri.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Laudate Dominum, quia bonus Dominus: psallite nomini eius, quoniam suave.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Quoniam Iacob elegit sibi Dominus Israel in possessionem sibi.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Quia ego cognovi quod magnus est Dominus, et Deus noster prae omnibus diis.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Omnia quaecumque voluit, Dominus fecit in caelo, in terra, in mari, et in omnibus abyssis.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Educens nubes ab extremo terrae: fulgura in pluviam fecit. Qui producit ventos de thesauris suis:
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 qui percussit primogenita Aegypti ab homine usque ad pecus.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Et misit signa, et prodigia in medio tui Aegypte: in Pharaonem, et in omnes servos eius.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Qui percussit gentes multas: et occidit reges fortes:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sehon regem Amorrhaeorum, et Og regem Basan, et omnia regna Chanaan.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 Et dedit terram eorum hereditatem, hereditatem Israel populo suo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Domine nomen tuum in aeternum: Domine memoriale tuum in generatione et generationem.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Quia iudicabit Dominus populum suum: et in servis suis deprecabitur.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Simulacra Gentium argentum, et aurum, opera manuum hominum.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Os habent, et non loquentur: oculos habent, et non videbunt.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Aures habent, et non audient: neque enim est spiritus in ore ipsorum.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Similes illis fiant qui faciunt ea: et omnes, qui confidunt in eis.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Domus Israel benedicite Domino: domus Aaron benedicite Domino.
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Domus Levi benedicite Domino: qui timetis Dominum, benedicite Domino.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Benedictus Dominus ex Sion, qui habitat in Ierusalem.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmorum 135 >