< Psalmorum 130 >

1 Canticum graduum. De profundis clamavi ad te Domine:
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Domine exaudi vocem meam: Fiant aures tuae intendentes, in vocem deprecationis meae.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Si iniquitates observaveris Domine: Domine quis sustinebit?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Quia apud te propitiatio est: et propter legem tuam sustinui te Domine. Sustinuit anima mea in verbo eius:
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 speravit anima mea in Domino.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 A custodia matutina usque ad noctem: speret Israel in Domino.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Quia apud Dominum misericordia: et copiosa apud eum redemptio.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Et ipse redimet Israel, ex omnibus iniquitatibus eius.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psalmorum 130 >