< Psalmorum 129 >

1 Canticum graduum. Saepe expugnaverunt me a iuventute mea, dicat nunc Israel.
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
2 Saepe expugnaverunt me a iuventute mea: etenim non potuerunt mihi.
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
3 Supra dorsum meum fabricaverunt peccatores: prolongaverunt iniquitatem suam.
Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
4 Dominus iustus concidet cervices peccatorum:
Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
5 confundantur et convertantur retrorsum omnes, qui oderunt Sion.
Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
6 Fiant sicut foenum tectorum: quod priusquam evellatur, exaruit:
Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
7 De quo non implebit manum suam qui metit, et sinum suum qui manipulos colligit.
ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
8 Et non dixerunt qui praeteribant: Benedictio Domini super vos: benediximus vobis in nomine Domini.
Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”

< Psalmorum 129 >