< Psalmorum 12 >

1 Psalmus David in finem, pro octava. Salvum me fac Domine, quoniam defecit sanctus: quoniam diminutae sunt veritates a filiis hominum.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2 Vana locuti sunt unusquisque ad proximum suum: labia dolosa, in corde et corde locuti sunt.
Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3 Disperdat Dominus universa labia dolosa, et linguam magniloquam.
Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
4 Qui dixerunt: Linguam nostram magnificabimus, labia nostra a nobis sunt, quis noster Dominus est?
ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
5 Propter miseriam inopum, et gemitum pauperum nunc exurgam, dicit Dominus. Ponam in salutari: fiducialiter agam in eo.
“Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
6 Eloquia Domini, eloquia casta: argentum igne examinatum, probatum terrae purgatum septuplum.
Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
7 Tu Domine servabis nos: et custodies nos a generatione hac in aeternum.
Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
8 In circuitu impii ambulant: secundum altitudinem tuam multiplicasti filios hominum.
Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

< Psalmorum 12 >