< Psalmorum 114 >

1 Alleluia. In exitu Israel de Aegypto, domus Iacob de populo barbaro:
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Facta est Iudaea sanctificatio eius, Israel potestas eius.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 Mare vidit, et fugit: Iordanis conversus est retrorsum.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 Montes exultaverunt ut arietes: et colles sicut agni ovium.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 Quid est tibi mare quod fugisti: et tu Iordanis, quia conversus es retrorsum?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 Montes exultastis sicut arietes, et colles sicut agni ovium?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 A facie Domini mota est terra, a facie Dei Iacob.
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 Qui convertit petram in stagna aquarum, et rupem in fontes aquarum.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psalmorum 114 >