< Psalmorum 112 >
1 Alleluia, conversio Aggaei, et Zachariae. Beatus vir, qui timet Dominum: in mandatis eius volet nimis.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Potens in terra erit semen eius: generatio rectorum benedicetur.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Gloria, et divitiae in domo eius: et iustitia eius manet in saeculum saeculi.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 Exortum est in tenebris lumen rectis: misericors, et miserator, et iustus.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 Iucundus homo qui miseretur et commodat, disponet sermones suos in iudicio:
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 quia in aeternum non commovebitur.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 In memoria aeterna erit iustus: ab auditione mala non timebit. Paratum cor eius sperare in Domino,
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 confirmatum est cor eius: non commovebitur donec despiciat inimicos suos.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 Dispersit, dedit pauperibus: iustitia eius manet in saeculum saeculi, cornu eius exaltabitur in gloria.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 Peccator videbit, et irascetur, dentibus suis fremet et tabescet: desiderium peccatorum peribit.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.