< Psalmorum 111 >

1 Alleluia. Confitebor tibi Domine in toto corde meo: in consilio iustorum, et congregatione.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 Magna opera Domini: exquisita in omnes voluntates eius.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 Confessio et magnificentia opus eius: et iustitia eius manet in saeculum saeculi.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 Memoriam fecit mirabilium suorum, misericors et miserator Dominus:
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 escam dedit timentibus se. Memor erit in saeculum testamenti sui:
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 virtutem operum suorum annunciabit populo suo:
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 Ut det illis hereditatem gentium: opera manuum eius veritas, et iudicium.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 Fidelia omnia mandata eius: confirmata in saeculum saeculi, facta in veritate et aequitate.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 Redemptionem misit populo suo: mandavit in aeternum testamentum suum. Sanctum, et terribile nomen eius:
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 initium sapientiae timor Domini. Intellectus bonus omnibus facientibus eum: laudatio eius manet in saeculum saeculi.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.

< Psalmorum 111 >