< Psalmorum 107 >

1 Alleluia alleluia. Confitemini Domino quoniam bonus: quoniam in saeculum misericordia eius.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Dicant qui redempti sunt a Domino, quos redemit de manu inimici: et de regionibus congregavit eos:
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 A solis ortu, et occasu: ab aquilone, et mari.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Erraverunt in solitudine in inaquoso: viam civitatis habitaculi non invenerunt,
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Esurientes, et sitientes: anima eorum in ipsis defecit.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum eripuit eos.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 Et deduxit eos in viam rectam: ut irent in civitatem habitationis.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Quia satiavit animam inanem: et animam esurientem satiavit bonis.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Sedentes in tenebris, et umbra mortis: vinctos in mendicitate, et ferro.
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Quia exacerbaverunt eloquia Dei: et consilium Altissimi irritaverunt.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Et humiliatum est in laboribus cor eorum: infirmati sunt, nec fuit qui adiuvaret.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Et eduxit eos de tenebris, et umbra mortis: et vincula eorum dirupit.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Quia contrivit portas aereas: et vectes ferreos confregit.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Suscepit eos de via iniquitatis eorum: propter iniustitias enim suas humiliati sunt.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Omnem escam abominata est anima eorum: et appropinquaverunt usque ad portas mortis.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur: et de necessitatibus eorum liberavit eos.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Misit verbum suum, et sanavit eos: et eripuit eos de interitionibus eorum.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Et sacrificent sacrificium laudis: et annuncient opera eius in exultatione.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Qui descendunt mare in navibus, facientes operationem in aquis multis.
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Ipsi viderunt opera Domini, et mirabilia eius in profundo.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Dixit, et stetit spiritus procellae: et exaltati sunt fluctus eius.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Ascendunt usque ad caelos, et descendunt usque ad abyssos: anima eorum in malis tabescebat.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Turbati sunt, et moti sunt sicut ebrius: et omnis sapientia eorum devorata est.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur, et de necessitatibus eorum eduxit eos.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Et statuit procellam eius in auram: et siluerunt fluctus eius.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Et laetati sunt quia siluerunt: et deduxit eos in portum voluntatis eorum.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Confiteantur Domino misericordiae eius: et mirabilia eius filiis hominum.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Et exaltent eum in ecclesia plebis: et in cathedra seniorum laudent eum.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Posuit flumina in desertum: et exitus aquarum in sitim.
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 Terram fructiferam in salsuginem, a malitia inhabitantium in ea.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Posuit desertum in stagna aquarum: et terram sine aqua in exitus aquarum.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Et collocavit illic esurientes: et constituerunt civitatem habitationis.
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 Et seminaverunt agros, et plantaverunt vineas: et fecerunt fructum nativitatis.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Et benedixit eis, et multiplicati sunt nimis: et iumenta eorum non minoravit.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Et pauci facti sunt: et vexati sunt a tribulatione malorum, et dolore.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Effusa est contentio super principes: et errare fecit eos in invio, et non in via.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Et adiuvit pauperem de inopia: et posuit sicut oves familias.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Videbunt recti, et laetabuntur: et omnis iniquitas oppilabit os suum.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Quis sapiens et custodiet haec? et intelliget misericordias Domini?
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Psalmorum 107 >