< Psalmorum 104 >

1 Psalmus David. Benedic anima mea Domino: Domine Deus meus magnificatus es vehementer. Confessionem, et decorem induisti:
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 amictus lumine sicut vestimento: Extendens caelum sicut pellem:
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 qui tegis aquis superiora eius. Qui ponis nubem ascensum tuum: qui ambulas super pennas ventorum.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Qui facis angelos tuos, spiritus: et ministros tuos ignem urentem.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Qui fundasti terram super stabilitatem suam: non inclinabitur in saeculum saeculi.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Abyssus, sicut vestimentum, amictus eius: super montes stabunt aquae.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 Ab increpatione tua fugient: a voce tonitrui tui formidabunt.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Ascendunt montes: et descendunt campi in locum, quem fundasti eis.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Terminum posuisti, quem non transgredientur: neque convertentur operire terram.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Qui emittis fontes in convallibus: inter medium montium pertransibunt aquae.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Potabunt omnes bestiae agri: expectabunt onagri in siti sua.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Super ea volucres caeli habitabunt: de medio petrarum dabunt voces.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Rigans montes de superioribus suis: de fructu operum tuorum satiabitur terra:
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Producens foenum iumentis, et herbam servituti hominum: Ut educas panem de terra:
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 et vinum laetificet cor hominis: Ut exhilaret faciem in oleo: et panis cor hominis confirmet.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Saturabuntur ligna campi, et cedri Libani, quas plantavit:
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 illic passeres nidificabunt. Herodii domus dux est eorum:
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 montes excelsi cervis: petra refugium herinaciis.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Fecit lunam in tempora: sol cognovit occasum suum.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Posuisti tenebras, et facta est nox: in ipsa pertransibunt omnes bestiae silvae.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Catuli leonum rugientes, ut rapiant, et quaerant a Deo escam sibi.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Ortus est sol, et congregati sunt: et in cubilibus suis collocabuntur.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Exibit homo ad opus suum: et ad operationem suam usque ad vesperum.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Quam magnificata sunt opera tua Domine! omnia in sapientia fecisti: impleta est terra possessione tua.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Hoc mare magnum, et spatiosum manibus: illic reptilia, quorum non est numerus. Animalia pusilla cum magnis:
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 illic naves pertransibunt. Draco iste, quem formasti ad illudendum ei:
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 omnia a te expectant ut des illis escam in tempore.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Dante te illis, colligent: aperiente te manum tuam, omnia implebuntur bonitate.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Avertente autem te faciem, turbabuntur: auferes spiritum eorum, et deficient, et in pulverem suum revertentur.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Emittes spiritum tuum, et creabuntur: et renovabis faciem terrae.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Sit gloria Domini in saeculum: laetabitur Dominus in operibus suis:
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Qui respicit terram, et facit eam tremere: qui tangit montes, et fumigant.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Cantabo Domino in vita mea: psallam Deo meo quamdiu sum.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Iucundum sit ei eloquium meum: ego vero delectabor in Domino.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Deficiant peccatores a terra, et iniqui ita ut non sint: benedic anima mea Domino.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psalmorum 104 >