< Proverbiorum 26 >

1 Quomodo nix in aestate, et pluviae in messe: sic indecens est stulto gloria.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Sicut avis ad alta transvolans, et passer quo libet vadens: sic maledictum frustra prolatum in quempiam superveniet.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Flagellum equo, et camus asino, et virga in dorso imprudentium.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Ne respondeas stulto iuxta stultitiam suam, ne efficiaris ei similis.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Responde stulto iuxta stultitiam suam, ne sibi sapiens esse videatur.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Claudus pedibus, et iniquitatem bibens, qui mittit verba per nuncium stultum.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Quomodo pulchras frustra habet claudus tibias: sic indecens est in ore stultorum parabola.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Sicut qui mittit lapidem in acervum Mercurii: ita qui tribuit insipienti honorem.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Quomodo si spina nascatur in manu temulenti: sic parabola in ore stultorum.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Iudicium determinat causas: et qui imponit stulto silentium, iras mitigat.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Sicut canis, qui revertitur ad vomitum suum, sic imprudens, qui iterat stultitiam suam.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Vidisti hominem sapientem sibi videri? magis illo spem habebit insipiens.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Dicit piger: Leo est in via, et leaena in itineribus:
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 sicut ostium vertitur in cardine suo, ita piger in lectulo suo.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Abscondit piger manum sub ascella sua, et laborat si ad os suum eam converterit.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Sapientior sibi piger videtur septem viris loquentibus sententias.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Sicut qui apprehendit auribus canem, sic qui transit impatiens, et commiscetur rixae alterius.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Sicut noxius est qui mittit sagittas, et lanceas in mortem:
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 ita vir, fraudulenter nocet amico suo: et cum fuerit deprehensus, dicit: Ludens feci.
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Cum defecerint ligna, extinguetur ignis: et susurrone subtracto, iurgia conquiescunt.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Sicut carbones ad prunas, et ligna ad ignem, sic homo iracundus suscitat rixas.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Verba susurronis quasi simplicia, et ipsa perveniunt ad intima ventris.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Quomodo si argento sordido ornare velis vas fictile, sic labia tumentia cum pessimo corde sociata.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Labiis suis intelligitur inimicus, cum in corde tractaverit dolos.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Quando submiserit vocem suam, ne credideris ei: quoniam septem nequitiae sunt in corde illius.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Qui operit odium fraudulenter, revelabitur malitia eius in consilio.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Qui fodit foveam, incidet in eam: et qui volvit lapidem, revertetur ad eum.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Lingua fallax non amat veritatem: et os lubricum operatur ruinas.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Proverbiorum 26 >