< Proverbiorum 25 >

1 Hae quoque parabolae Salomonis, quas transtulerunt viri Ezechiae regis Iuda.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 Gloria Dei est celare verbum, et gloria regum investigare sermonem.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Caelum sursum, et terra deorsum, et cor regum inscrutabile.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Aufer rubiginem de argento, et egredietur vas purissimum:
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Aufer impietatem de vultu regis, et firmabitur iustitia thronus eius.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Ne gloriosus appareas coram rege, et in loco magnorum ne steteris.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Melius est enim ut dicatur tibi: Ascende huc; quam ut humilieris coram principe.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Quae viderunt oculi tui, ne proferas in iurgio cito: ne postea emendare non possis, cum dehonestaveris amicum tuum.
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Causam tuam tracta cum amico tuo, et secretum extraneo ne reveles:
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 ne forte insultet tibi cum audierit, et exprobrare non cesset. Gratia et amicitia liberant: quas tibi serva, ne exprobrabilis fias.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Mala aurea in lectis argenteis, qui loquitur verbum in tempore suo.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Inauris aurea, et margaritum fulgens, qui arguit sapientem, et aurem obedientem.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Sicut frigus nivis in die messis, ita legatus fidelis ei, qui misit eum, animam ipsius requiescere facit.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Nubes, et ventus, et pluviae non sequentes, vir gloriosus, et promissa non complens.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Patientia lenietur princeps, et lingua mollis confringet duritiam.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Mel invenisti, comede quod sufficit tibi, ne forte satiatus evomas illud.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Subtrahe pedem tuum de domo proximi tui, nequando satiatus oderit te.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Iaculum, et gladius, et sagitta acuta, homo qui loquitur contra proximum suum falsum testimonium.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Dens putridus, et pes lassus, qui sperat super infideli in die angustiae,
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 et amittit pallium in die frigoris. Acetum in nitro, qui cantat carmina cordi pessimo. Sicut tinea vestimento, et vermis ligno: ita tristitia viri nocet cordi.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Si esurierit inimicus tuus, ciba illum: si sitierit, da ei aquam bibere:
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 prunas enim congregabis super caput eius, et Dominus reddet tibi.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Ventus aquilo dissipat pluvias, et facies tristis linguam detrahentem.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Aqua frigida animae sitienti, et nuncius bonus de terra longinqua.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Fons turbatus pede, et vena corrupta, iustus cadens coram impio.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Sicut qui mel multum comedit, non est ei bonum: sic qui scrutator est maiestatis, opprimetur a gloria.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Sicut urbs patens et absque murorum ambitu, ita vir, qui non potest in loquendo cohibere spiritum suum.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Proverbiorum 25 >