< Proverbiorum 22 >
1 Melius est nomen bonum, quam divitiae multae: super argentum et aurum, gratia bona.
Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 Dives, et pauper obviaverunt sibi: utriusque operator est Dominus.
Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 Callidus videt malum, et abscondit se: innocens pertransiit, et afflictus est damno.
Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 Finis modestiae timor Domini, divitiae et gloria et vita.
Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 Arma et gladii in via perversi: custos autem animae suae longe recedit ab eis.
Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 Proverbium est: Adolescens iuxta viam suam, etiam cum senuerit, non recedet ab ea.
Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7 Dives pauperibus imperat: et qui accipit mutuum, servus est foenerantis.
Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8 Qui seminat iniquitatem, metet mala, et virga irae suae consummabitur.
Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9 Qui pronus est ad misericordiam, benedicetur: de panibus enim suis dedit pauperi. Victoriam et honorem acquiret qui dat munera: animam autem aufert accipientium.
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10 Eiice derisorem, et exibit cum eo iurgium, cessabuntque causae et contumeliae.
Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11 Qui diligit cordis munditiam, propter gratiam labiorum suorum habebit amicum regem.
Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12 Oculi Domini custodiunt scientiam: et supplantantur verba iniqui.
Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13 Dicit piger: Leo est foris, in medio platearum occidendus sum.
Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14 Fovea profunda, os alienae: cui iratus est Dominus, incidet in eam.
Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15 Stultitia colligata est in corde pueri, et virga disciplinae fugabit eam.
Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16 Qui calumniatur pauperem, ut augeat divitias suas, dabit ipse ditiori, et egebit.
Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17 Fili mi! Inclina aurem tuam, et audi verba sapientium: appone autem cor ad doctrinam meam.
Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18 quae pulchra erit tibi, cum servaveris eam in ventre tuo, et redundabit in labiis tuis:
maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19 Ut sit in Domino fiducia tua, unde et ostendi eam tibi hodie.
Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20 Ecce descripsi eam tibi tripliciter, in cogitationibus et scientia:
Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21 ut ostenderem tibi firmitatem, et eloquia veritatis, respondere ex his illis, qui miserunt te.
kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22 Non facias violentiam pauperi, quia pauper est: neque conteras egenum in porta:
Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23 quia iudicabit Dominus causam eius, et configet eos, qui confixerunt animam eius.
maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24 Noli esse amicus homini iracundo, neque ambules cum viro furioso:
Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25 ne forte discas semitas eius, et sumas scandalum animae tuae.
au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
26 Noli esse cum his, qui defigunt manus suas, et qui vades se offerunt pro debitis:
Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
27 si enim non habes unde restituas, quid causae est ut tollat operimentum de cubili tuo?
Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
28 Ne transgrediaris terminos antiquos, quos posuerunt patres tui.
Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
29 Vidisti virum velocem in opere suo? coram regibus stabit, nec erit ante ignobiles.
Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.