< Proverbiorum 21 >

1 Sicut divisiones aquarum, ita cor regis in manu Domini: quocumque voluerit, inclinabit illud.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Omnis via viri recta sibi videtur: appendit autem corda Dominus.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Facere misericordiam et iudicium, magis placet Domino quam victimae.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Exaltatio oculorum est dilatatio cordis: lucerna impiorum peccatum.
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5 Cogitationes robusti semper in abundantia: omnis autem piger semper in egestate est.
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Qui congregat thesauros lingua mendacii, vanus et excors est, et impingetur ad laqueos mortis.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 Rapinae impiorum detrahent eos, quia noluerunt facere iudicium.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 Perversa via viri, aliena est: qui autem mundus est, rectum opus eius.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 Melius est sedere in angulo domatis, quam cum muliere litigiosa, et in domo communi.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 Anima impii desiderat malum, non miserebitur proximo suo.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 Mulctato pestilente sapientior erit parvulus: et si sectetur sapientem, sumet scientiam.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 Excogitat iustus de domo impii, ut detrahat impios a malo.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 Qui obturat aurem suam ad clamorem pauperis, et ipse clamabit, et non exaudietur.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 Munus absconditum extinguit iras: et donum in sinu indignationem maximam.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 Gaudium iusto est facere iudicium: et pavor operantibus iniquitatem.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 Vir, qui erraverit a via doctrinae, in coetu gigantum commorabitur.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 Qui diligit epulas, in egestate erit: qui amat vinum, et pinguia, non ditabitur.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 Pro iusto dabitur impius: et pro rectis iniquus.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 Melius est habitare in terra deserta, quam cum muliere rixosa et iracunda.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 Thesaurus desiderabilis, et oleum in habitaculo iusti: et imprudens homo dissipabit illud.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 Qui sequitur iustitiam et misericordiam, inveniet vitam, et gloriam.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 Civitatem fortium ascendit sapiens, detraxitque robur fiduciae eius.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 Qui custodit os suum, et linguam suam, custodit ab angustiis animam suam.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 Superbus et arrogans vocatur indoctus, qui in ira operatur superbiam.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 Desideria occidunt pigrum: noluerunt enim quidquam manus eius operari:
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 tota die concupiscit et desiderat: qui autem iustus est, tribuet, et non cessabit.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 Hostiae impiorum abominabiles, quae offeruntur ex scelere.
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 Testis mendax peribit: vir obediens loquetur victoriam.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 Vir impius procaciter obfirmat vultum suum: qui autem rectus est, corrigit viam suam.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 Non est sapientia, non est prudentia, non est consilium contra Dominum.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 Equus paratur ad diem belli: Dominus autem salutem tribuit.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Proverbiorum 21 >