< Proverbiorum 11 >

1 Statera dolosa, abominatio est apud Deum: et pondus aequum, voluntas eius.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 Ubi fuerit superbia, ibi erit et contumelia: ubi autem est humilitas, ibi et sapientia.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 Simplicitas iustorum diriget eos: et supplantatio perversorum vastabit illos.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 Non proderunt divitiae in die ultionis: iustitia autem liberabit a morte.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 Iustitia simplicis diriget viam eius: et in impietate sua corruet impius.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 Iustitia rectorum liberabit eos: et in insidiis suis capientur iniqui.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 Mortuo homine impio, nulla erit ultra spes: et expectatio solicitorum peribit.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 Iustus de angustia liberatus est: et tradetur impius pro eo.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 Simulator ore decipit amicum suum: iusti autem liberabuntur scientia.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 In bonis iustorum exultabit civitas: et in perditione impiorum erit laudatio.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 Benedictione iustorum exaltabitur civitas: et ore impiorum subvertetur.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 Qui despicit amicum suum, indigens corde est: vir autem prudens tacebit.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 Qui ambulat fraudulenter, revelat arcana: qui autem fidelis est, celat amici commissum.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Ubi non est gubernator, populus corruet: salus autem, ubi multa consilia.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 Affligetur malo, qui fidem facit pro extraneo: qui autem cavet laqueos, securus erit.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 Mulier gratiosa inveniet gloriam: et robusti habebunt divitias.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 Benefacit animae suae vir misericors: qui autem crudelis est, etiam propinquos abiicit.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 Impius facit opus instabile: seminanti autem iustitiam merces fidelis.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 Clementia praeparat vitam: et sectatio malorum mortem.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 Abominabile Domino cor pravum: et voluntas eius in iis, qui simpliciter ambulant.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 Manus in manu non erit innocens malus: semen autem iustorum salvabitur.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 Circulus aureus in naribus suis, mulier pulchra et fatua.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 Desiderium iustorum omne bonum est: praestolatio impiorum furor.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 Alii dividunt propria, et ditiores fiunt: alii rapiunt non sua, et semper in egestate sunt.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 Anima, quae benedicit, impinguabitur: et qui inebriat, ipse quoque inebriabitur.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 Qui abscondit frumenta, maledicetur in populis: benedictio autem super caput vendentium.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 Bene consurgit diluculo qui quaerit bona: qui autem investigator malorum est, opprimetur ab eis.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 Qui confidit in divitiis suis, corruet: iusti autem quasi virens folium germinabunt.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 Qui conturbat domum suam, possidebit ventos: et qui stultus est, serviet sapienti.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 Fructus iusti lignum vitae: et qui suscipit animas, sapiens est.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Si iustus in terra recipit, quanto magis impius et peccator?
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Proverbiorum 11 >