< Proverbiorum 10 >

1 Filius sapiens laetificat patrem: filius vero stultus moestitia est matris suae.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Nil proderunt thesauri impietatis: iustitia vero liberabit a morte.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Non affliget Dominus fame animam iusti, et insidias impiorum subvertet.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 Egestatem operata est manus remissa: manus autem fortium divitias parat. Qui nititur mendaciis, hic pascit ventos: idem autem ipse sequitur aves volantes.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Qui congregat in messe, filius sapiens est: qui autem stertit aestate, filius confusionis.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Benedictio Domini super caput iusti: os autem impiorum operit iniquitas.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 Memoria iusti cum laudibus: et nomen impiorum putrescet.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Sapiens corde praecepta suscipit: stultus caeditur labiis.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Qui ambulat simpliciter, ambulat confidenter: qui autem depravat vias suas, manifestus erit.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 Qui annuit oculo, dabit dolorem: et stultus labiis verberabitur.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 Vena vitae, os iusti: et os impiorum operit iniquitatem.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Odium suscitat rixas: et universa delicta operit charitas.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 In labiis sapientis invenitur sapientia: et virga in dorso eius qui indiget corde.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Sapientes abscondunt scientiam: os autem stulti confusioni proximum est.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 Substantia divitis, urbs fortitudinis eius: pavor pauperum, egestas eorum.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 Opus iusti ad vitam: fructus autem impii ad peccatum.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 Via vitae, custodienti disciplinam: qui autem increpationes relinquit, errat.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Abscondunt odium labia mendacia: qui profert contumeliam, insipiens est.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 In multiloquio non deerit peccatum: qui autem moderatur labia sua prudentissimus est.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 Argentum electum, lingua iusti: cor autem impiorum pro nihilo.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Labia iusti erudiunt plurimos: qui autem indocti sunt, in cordis egestate morientur.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 Benedictio Domini divites facit, nec sociabitur eis afflictio.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 Quasi per risum stultus operatur scelus: sapientia autem est viro prudentia.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 Quod timet impius, veniet super eum: desiderium suum iustus dabitur.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Quasi tempestas transiens non erit impius: iustus autem quasi fundamentum sempiternum.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Sicut acetum dentibus, et fumus oculis, sic piger his, qui miserunt eum.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Timor Domini apponet dies: et anni impiorum breviabuntur.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 Expectatio iustorum laetitia: spes autem impiorum peribit.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 Fortitudo simplicis via Domini: et pavor his, qui operantur malum.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Iustus in aeternum non commovebitur: impii autem non habitabunt super terram.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 Os iusti parturiet sapientiam: lingua pravorum peribit.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Labia iusti considerant placita: et os impiorum perversa.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Proverbiorum 10 >