< Philemonem 1 >
1 Paulus vinctus Christi Iesu, et Timotheus frater: Philemoni dilecto, et adiutori nostro,
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
2 et Apiae sorori charissimae, et Archippo commilitoni nostro, et Ecclesiae, quae in domo tua est.
na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
3 Gratia vobis, et pax a Deo Patre nostro, et Domino Iesu Christo.
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
4 Gratias ago Deo meo, semper memoriam tui faciens in orationibus meis,
Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
5 audiens charitatem tuam, et fidem, quam habes in Domino Iesu, et in omnes sanctos:
Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
6 ut communicatio fidei tuae evidens fiat in agnitione omnis operis boni, quod est in vobis in Christo Iesu.
Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
7 Gaudium enim magnum habui, et consolationem in charitate tua: quia viscera sanctorum requieverunt per te, frater.
Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
8 Propter quod multam fiduciam habens in Christo Iesu imperandi tibi quod ad rem pertinet:
Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
9 propter charitatem magis obsecro, cum sis talis, ut Paulus senex, nunc autem et vinctus Iesu Christi:
lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
10 Obsecro te pro meo filio, quem genui in vinculis, Onesimo,
Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
11 qui tibi aliquando inutilis fuit, nunc autem et mihi, et tibi utilis,
Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
12 quem remisi tibi. Tu autem illum, ut mea viscera, suscipe:
Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
13 quem ego volueram mecum detinere, ut pro te mihi ministraret in vinculis Evangelii:
Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
14 sine consilio autem tuo nihil volui facere, uti ne velut ex necessitate bonum tuum esset, sed voluntarium.
Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
15 Forsitan enim ideo discessit ad horam a te, ut in aeternum illum reciperes: (aiōnios )
Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios )
16 iam non ut servum, sed pro servo charissimum fratrem, maxime mihi: quanto autem magis tibi et in carne, et in Domino?
Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
17 Si ergo habes me socium, suscipe illum sicut me:
Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
18 Si autem aliquid nocuit tibi, aut debet: hoc mihi imputa.
Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
19 Ego Paulus scripsi mea manu: ego reddam, ut non dicam tibi, quod et teipsum mihi debes:
Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
20 ita facies. Ego te fruar in Domino: Refice viscera mea in Christo.
Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 Confidens in obedientia tua scripsi tibi: sciens quoniam et super id, quod dico, facies.
Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
22 Simul autem et para mihi hospitium: nam spero per orationes vestras donari me vobis.
Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
23 Salutat te Epaphras concaptivus meus in Christo Iesu,
Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
24 Marcus, Aristarchus, Demas, et Lucas, adiutores mei.
na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
25 Gratia Domini nostri Iesu Christi cum spiritu vestro. Amen.
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.