< Liber Numeri 33 >

1 Hae sunt mansiones filiorum Israel, qui egressi sunt de Aegypto per turmas suas in manu Moysi et Aaron,
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 quas descripsit Moyses iuxta castrorum loca, quae Domini iussione mutabant.
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Profecti igitur de Ramesse mense primo, quintadecima die mensis primi, fecerunt altera die Phase filii Israel in manu excelsa videntibus cunctis Aegyptiis,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 et sepelientibus primogenitos, quos percusserat Dominus (nam et in diis eorum exercuerat ultionem)
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 castrametati sunt in Soccoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Et de Soccoth venerunt in Etham, quae est in extremis finibus solitudinis.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Inde egressi venerunt contra Phihahiroth, quae respicit Beelsephon, et castrametati sunt ante Magdalum.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Profectique de Phihahiroth, transierunt per medium mare in solitudinem: et ambulantes tribus diebus per desertum Etham, castrametati sunt in Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Profectique de Mara venerunt in Elim, ubi erant duodecim fontes aquarum, et palmae septuaginta: ibique castrametati sunt.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Sed et inde egressi, fixerunt tentoria super Mare rubrum. Profectique de Mari rubro,
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 castrametati sunt in deserto Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Unde egressi, venerunt in Daphca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Profectique de Daphca, castrametati sunt in Alus.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Egressique de Alus, in Raphidim fixere tentoria, ubi populo defuit aqua ad bibendum.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Profectique de Raphidim, castrametati sunt in deserto Sinai.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Sed et de solitudine Sinai egressi, venerunt ad sepulchra concupiscentiae.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Profectique de sepulchris concupiscentiae, castrametati sunt in Haseroth.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Et de Haseroth venerunt in Rethma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Profectique de Rethma, castrametati sunt in Remmomphares.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Unde egressi venerunt in Lebna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 De Lebna castrametati sunt in Ressa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Egressique de Ressa, venerunt in Ceelatha.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Unde profecti castrametati sunt in monte Sepher.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Egressi de monte Sepher, venerunt in Arada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Inde proficiscentes, castrametati sunt in Maceloth.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Profectique de Maceloth, venerunt in Thahath.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 De Thahath castrametati sunt in Thare.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Unde egressi, fixere tentoria in Methca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Et de Methca castrametati sunt in Hesmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Profectique de Hesmona, venerunt in Moseroth.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Et de Moseroth castrametati sunt in Beneiaacan.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Profectique de Beneiaacan, venerunt in montem Gadgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Unde profecti, castrametati sunt in Ietebatha.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Et de Ietebatha venerunt in Hebrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Egressique de Hebrona, castrametati sunt in Asiongaber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Inde profecti, venerunt in desertum Sin, haec est Cades.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Egressique de Cades, castrametati sunt in monte Hor, in extremis finibus Terrae Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Ascenditque Aaron sacerdos in montem Hor iubente Domino: et ibi mortuus est anno quadragesimo egressionis filiorum Israel ex Aegypto, mense quinto, prima die mensis,
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 cum esset annorum centum viginti trium.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Audivitque Chananaeus rex Arad, qui habitabat ad meridiem, in Terram Chanaan venisse filios Israel.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Et profecti de monte Hor, castrametati sunt in Salmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Unde egressi, venerunt in Phunon.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Profectique de Phunon, castrametati sunt in Oboth.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Et de Oboth, venerunt in Ieabarim, quae est in finibus Moabitarum.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Profectique de Ieabarim, fixere tentoria in Dibongad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Unde egressi, castrametati sunt in Helmondeblathaim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Egressique de Helmondeblathaim, venerunt ad montes Abarim contra Nabo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Profectique de montibus Abarim, transierunt ad campestria Moab, supra Iordanem contra Iericho.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Ibique castrametati sunt de Bethsimoth usque ad Abelsatim in planioribus locis Moabitarum,
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 ubi locutus est Dominus ad Moysen:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Praecipe filiis Israel, et dic ad eos: Quando transieritis Iordanem, intrantes Terram Chanaan,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 disperdite cunctos habitatores Terrae illius: confringite titulos, et statuas comminuite, atque omnia excelsa vastate,
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 mundantes terram, et habitantes in ea. ego enim dedi vobis illam in possessionem,
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 quam dividetis vobis sorte. Pluribus dabitis latiorem, et paucioribus angustiorem. Singulis ut sors ceciderit, ita tribuetur hereditas. Per tribus et familias possessio dividetur.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Sin autem nolueritis interficere habitatores Terrae: qui remanserint, erunt vobis quasi clavi in oculis, et lanceae in lateribus, et adversabuntur vobis in Terra habitationis vestrae:
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 et quidquid illis cogitaveram facere, vobis faciam.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Liber Numeri 33 >