< Liber Numeri 1 >

1 Locutusque est Dominus ad Moysen in deserto Sinai in tabernaculo foederis, prima die mensis secundi, anno altero egressionis eorum ex Aegypto, dicens:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Tollite summam universae congregationis filiorum Israel per cognationes et domos suas, et nomina singulorum, quidquid sexus est masculini
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 a vigesimo anno et supra, omnium virorum fortium ex Israel, et numerabitis eos per turmas suas, tu et Aaron.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 Eruntque vobiscum principes tribuum ac domorum in cognationibus suis,
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 quorum ista sunt nomina: De Ruben, Elisur filius Sedeur.
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 de Simeon, Salamiel filius Surisaddai.
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 de Iuda, Nahasson, filius Aminadab.
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 de Issachar, Nathanael filius Suar.
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 de Zabulon, Eliab filius Helon.
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 Filiorum autem Ioseph, de Ephraim, Elisama filius Ammiud. de Manasse, Gamaliel filius Phadasseur.
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 De Beniamin, Abidan filius Gedeonis.
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 de Dan, Ahiezer filius Ammisaddai.
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 de Aser, Phegiel filius Ochran.
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 de Gad, Eliasaph filius Duel.
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 de Nephthali, Ahira filius Enan.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Hi nobilissimi principes multitudinis per tribus et cognationes suas, et capita exercitus Israel:
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 quos tulerunt Moyses et Aaron cum omni vulgi multitudine:
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 et congregaverunt primo die mensis secundi, recensentes eos per cognationes, et domos, ac familias, et capita, et nomina singulorum a vigesimo anno et supra,
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 sicut praeceperat Dominus Moysi. Numeratique sunt in deserto Sinai.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 De Ruben primogenito Israelis per generationes et familias ac domos suas, et nomina capitum singulorum, omne quod sexus est masculini a vigesimo anno et supra, procedentium ad bellum,
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 quadraginta sex millia quingenti.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 De filiis Simeon per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina et capita singulorum, omne quod sexus est masculini a vigesimo anno et supra, procedentium ad bellum,
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 quinquaginta novem millia trecenti.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 De filiis Gad per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a viginti annis et supra, omnes qui ad bella procederent,
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 quadragintaquinque millia sexcenti quinquaginta.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 De filiis Iuda per generationes et familias ac domos cognationum suarum, per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 recensiti sunt septuaginta quattuor millia sexcenti.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 De filiis Issachar, per generationes et familias ac domos cognationum suarum, per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui ad bella procederent,
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 recensiti sunt quinquaginta quattuor millia quadringenti.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 De filiis Zabulon per generationes et familias, ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 quinquaginta septem millia quadringenti.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 De filiis Ioseph, filiorum Ephraim per generationes, et familias, ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 quadraginta millia quingenti.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Porro filiorum Manasse per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a viginti annis et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 triginta duo millia ducenti.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 De filiis Beniamin per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 triginta quinque millia quadringenti.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 De filiis Dan per generationes, et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 sexaginta duo millia septingenti.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 De filiis Aser per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt per nomina singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 quadraginta millia et mille quingenti.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 De filiis Nephthali per generationes et familias ac domos cognationum suarum recensiti sunt nominibus singulorum a vigesimo anno et supra, omnes qui poterant ad bella procedere,
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 quinquaginta tria millia quadringenti.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Hi sunt, quos numeraverunt Moyses et Aaron, et duodecim principes Israel, singulos per domos cognationum suarum.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 Fueruntque omnis numerus filiorum Israel per domos et familias suas a vigesimo anno et supra, qui poterant ad bella procedere,
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 sexcenta tria millia virorum quingenti quinquaginta.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Levitae autem in tribu familiarum suarum non sunt numerati cum eis.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Locutusque est Dominus ad Moysen, dicens:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Tribum Levi noli numerare, neque pones summam eorum cum filiis Israel:
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 sed constitue eos super tabernaculum testimonii et cuncta vasa eius, et quidquid ad ceremonias pertinet. Ipsi portabunt tabernaculum et omnia utensilia eius: et erunt in ministerio, ac per gyrum tabernaculi metabuntur.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 Cum proficiscendum fuerit, deponent Levitae tabernaculum: cum castrametanda, erigent. quisquis externorum accesserit, occidetur.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 Metabuntur autem castra filii Israel unusquisque per turmas et cuneos atque exercitum suum.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Porro Levitae per gyrum tabernaculi figent tentoria, ne fiat indignatio super multitudinem filiorum Israel, et excubabunt in custodiis tabernaculi testimonii.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Fecerunt ergo filii Israel iuxta omnia quae praeceperat Dominus Moysi.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Liber Numeri 1 >