< Nehemiæ 7 >

1 Postquam autem aedificatus est murus, et posui valvas, et recensui ianitores, et cantores, et Levitas:
Baada ya ukuta kukamilika kujengwa upya na nikaweka milango, mabawabu wa lango, waimbaji, na Walawi waliteuliwa.
2 praecepi Hanani fratri meo, et Hananiae principi domus de Ierusalem (ipse enim quasi vir verax et timens Deum plus ceteris videbatur)
Nikamweka Hanani ndugu yangu kuwa kiongozi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwadilifu na mwenye kumcha Mungu kuliko watu wengine.
3 et dixi eis: Non aperiantur portae Ierusalem usque ad calorem solis. Cumque adhuc assisterent, clausae portae sunt, et oppilatae: et posui custodes de habitatoribus Ierusalem, singulos per vices suas, et unumquemque contra domum suam.
Nikawaambia, “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka jua litakapokuwa limepanda. Walinzi wa malango wakiwa bado kwenye zamu, waamuru wafunge milango na waweke makomeo. Pia wateueni wenyeji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja kwenye lindo lake, na wengine karibu na nyumba zao wenyewe.”
4 Civitas autem erat lata nimis et grandis, et populus parvus in medio eius, et non erant domus aedificatae.
Mji ulikuwa mkubwa, tena wenye nafasi nyingi, lakini walikuwepo watu wachache ndani yake, nazo nyumba zilikuwa bado ni magofu.
5 Deus autem dedit in corde meo, et congregavi optimates, et magistratus, et vulgus, ut recenserem eos: et inveni librum census eorum, qui ascenderant primum, et inventum est scriptum in eo.
Hivyo Mungu wangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, maafisa na watu wa kawaida kwa ajili ya kuorodheshwa kulingana na jamaa zao. Nilikuta orodha ya vizazi ya wale waliokuwa wa kwanza kurudi toka utumwani. Haya ndiyo niliyokuta yameandikwa humo:
6 Isti filii provinciae, qui ascenderunt de captivitate migrantium, quos transtulerat Nabuchodonosor rex Babylonis, et reversi sunt in Ierusalem, et in Iudaeam, unusquisque in civitatem suam.
Hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
7 Qui venerunt cum Zorobabel, Iosue, Nehemias, Azarias, Raamias, Nahamani, Mardochaeus, Belsam, Mespharath, Begoai, Nahum, Baana. Numerus virorum populi Israel:
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu na Baana): Orodha ya wanaume wa Israeli ilikuwa:
8 Filii Pharos, duo millia centum septuaginta duo:
wazao wa Paroshi 2,172
9 Filii Saphatia, trecenti septuaginta duo:
wazao wa Shefatia 372
10 Filii Area, sexcenti quinquaginta duo:
wazao wa Ara 652
11 Filii Phahathmoab filiorum Iosue et Ioab, duo millia octingenti decem et octo:
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,818
12 Filii Aelam, mille octigenti quinquagintaquattuor:
wazao wa Elamu 1,254
13 Filii Zethua, octingenti quadragintaquinque:
wazao wa Zatu 845
14 Filii Zachai, septingenti sexaginta:
wazao wa Zakai 760
15 Filii Bannui, sexcenti quadragintaocto:
wazao wa Binui 648
16 Filii Bebai, sexcenti vigintiocto:
wazao wa Bebai 628
17 Filii Azgad, duo millia trecenti vigintiduo:
wazao wa Azgadi 2,322
18 Filii Adonicam, sexcenti sexagintaseptem:
wazao wa Adonikamu 667
19 Filii Beguai, duo millia sexagintaseptem:
wazao wa Bigwai 2,067
20 Filii Adin, sexcenti quinquagintaquinque:
wazao wa Adini 655
21 Filii Ater, filii Hezeciae, nonagintaocto:
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
22 Filii Hasem, trecenti vigintiocto:
wazao wa Hashumu 328
23 Filii Besai, trecenti vigintiquattuor:
wazao wa Besai 324
24 Filii Hareph, centum duodecim:
wazao wa Harifu 112
25 Filii Gabaon, nonagintaquinque:
wazao wa Gibeoni 95
26 Filii Bethlehem, et Netupha, centum octogintaocto.
watu wa Bethlehemu na Netofa 188
27 Viri Anathoth, centum vigintiocto.
watu wa Anathothi 128
28 Viri Bethazmoth, quadragintaduo.
watu wa Beth-Azmawethi 42
29 Viri Cariathiarim, Cephira, et Beroth, septingenti quadragintatres.
watu wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
30 Viri Rama et Geba, sexcenti vigintiunus.
watu wa Rama na Geba 621
31 Viri Machmas, centum vigintiduo.
watu wa Mikmashi 122
32 Viri Bethel et Hai, centum vigintitres.
watu wa Betheli na Ai 123
33 Viri Nebo alterius, quinquagintaduo.
watu wa Nebo 52
34 Viri Aelam alterius, mille ducenti quinquagintaquattuor.
wazao wa Elamu 1,254
35 Filii Harem, trecenti viginti.
wazao wa Harimu 320
36 Filii Iericho, trecenti quadragintaquinque.
wazao wa Yeriko 345
37 Filii Lod Hadid et Ono, septingenti vigintiunus.
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 721
38 Filii Senaa, tria millia nongenti triginta.
wazao wa Senaa 3,930
39 Sacerdotes: Filii Idaia in domo Iosue, nongenti septuagintatres.
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
40 Filii Emmer, mille quinquagintaduo.
wazao wa Imeri 1,052
41 Filii Phashur, mille ducenti quadragintaseptem.
wazao wa Pashuri 1,247
42 Filii Arem, mille decem et septem. Levitae:
wazao wa Harimu 1,017
43 Filii Iosue et Cedmihel filiorum
Walawi: wazao wa Yeshua (kupitia Kadmieli kupitia jamaa ya Hodavia) 74
44 Oduiae, septuagintaquattuor. Cantores:
Waimbaji: wazao wa Asafu 148
45 Filii Asaph, centum quadragintaocto.
Mabawabu wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 138
46 Ianitores: filii Sellum, filii Ater, filii Telmon, filii Accub, filii Hatita, filii Sobai: centum trigintaocto.
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
47 Nathinaei: filii Soha, filii Hasupha, filii Tebbaoth,
wazao wa Kerosi, Sia, Padoni,
48 filii Ceros, filii Siaa, filii Phadon, filii Lebana, filii Hagaba, filii Selmai,
wazao wa Lebana, Hagaba, Shalmai,
49 filii Hanan, filii Geddel, filii Gaher,
wazao wa Hanani, Gideli, Gahari,
50 filii Raaia, filii Rasin, filii Necoda,
wazao wa Reaya, Resini, Nekoda,
51 filii Gezem, filii Aza, filii Phasea,
wazao wa Gazamu, Uza, Pasea,
52 filii Besai, filii Munim, filii Nephussim,
wazao wa Besai, Meunimu, Nefusimu,
53 filii Bacbuc, filii Hacupha, filii Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
54 filii Besloth, filii Mahida, filii Harsa,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
55 filii Bercos, filii Sisara, filii Thema,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
56 filii Nasia, filii Hatipha,
wazao wa Nesia na Hatifa.
57 filii servorum Salomonis, filii Sothai, filii Sophereth, filii Pharida,
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Soferethi, Perida,
58 filii Iahala, filii Darcon, filii Ieddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
59 filii Saphatia, filii Hatil, filii Phochereth, qui erat ortus ex Sabaim, filio Amon.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Amoni.
60 Omnes Nathinaei, et filii servorum Salomonis, trecenti nonagintaduo.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
61 Hi sunt autem, qui ascenderunt de Thelmela, Thelharsa, Cherub, Addon, et Emmer: et non potuerunt indicare domum patrum suorum, et semen suum, utrum ex Israel essent.
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
62 Filii Dalaia, filii Tobia, filii Necoda, sexcenti quadragintaduo.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 642
63 Et de Sacerdotibus, filii Habia, filii Accos, filii Berzellai, qui accepit de filiabus Berzellai Galaaditis uxorem: et vocatus est nomine eorum.
Na kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi na Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
64 Hi quaesierunt scripturam suam in censu, et non invenerunt: et eiecti sunt de sacerdotio.
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani, kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
65 Dixitque Athersatha eis ut non manducarent de Sanctis sanctorum, donec staret Sacerdos doctus et eruditus.
Kwa hiyo, mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
66 Omnis multitudo quasi vir unus quadragintaduo millia sexcenti sexaginta,
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
67 absque servis et ancillis eorum, qui erant septem millia trecenti trigintaseptem, et inter eos cantores, et cantatrices, ducenti quadragintaquinque.
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 245.
68 Equi eorum, septingenti trigintasex: muli eorum, ducenti quadragintaquinque:
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245
69 cameli eorum, quadringenti trigintaquinque: asini, sex millia septingenti viginti.
ngamia 435 na punda 6,720.
70 Nonnulli autem de principibus familiarum dederunt in opus. Athersatha dedit in thesaurum auri drachmas mille, phialas quinquaginta, tunicas sacerdotales quingentas triginta.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walichangia kazi ya ujenzi. Mtawala alikabidhi kwenye hazina darkoni 1,000 za dhahabu, mabakuli 50, na mavazi 530 kwa ajili ya makuhani.
71 Et de principibus familiarum dederunt in thesaurum operis auri drachmas viginti millia, et argenti mnas duo millia ducentas.
Baadhi ya viongozi wa jamaa walikabidhi kwenye hazina darkoni 20,000 za dhahabu, na mane 2,200 za fedha kwa ajili ya kazi hiyo.
72 Et quod dedit reliquus populus, auri drachmas viginti millia, et argenti mnas duo millia, et tunicas sacerdotales sexagintaseptem.
Jumla ya matoleo ya watu wengine yalikuwa ni darkoni 20,000 za dhahabu, mane 2,000 za fedha, na mavazi sitini na saba ya makuhani.
73 Habitaverunt autem Sacerdotes, et Levitae, et ianitores, et cantores, et reliquum vulgus, et Nathinaei, et omnis Israel in civitatibus suis.
Makuhani, Walawi, mabawabu, waimbaji na watumishi wa Hekalu, pamoja na baadhi ya watu wengine na Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao wenyewe. Ilipotimia miezi saba, nao Waisraeli wakiwa tayari wanaishi katika miji yao,

< Nehemiæ 7 >