< Iosue 12 >
1 Hi sunt reges, quos percusserunt filii Israel, et possederunt Terram eorum trans Iordanem ad solis ortum, a torrente Arnon usque ad montem Hermon, et omnem Orientalem plagam, quae respicit solitudinem.
Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao watu wa Israeli walishindwa. Waisraeli walichukua miliki ya nchi katika upande wa mashariki mwa Yordani sehemu ambako jua huchomoza, kutoka bonde la Mto Arnoni hadi Mlima Hermoni, na nchi yote ya Araba kuelekea kusini.
2 Sehon rex Amorrhaeorum, qui habitavit in Hesebon, dominatus est ab Aroer, quae sita est super ripam torrentis Arnon, et mediae partis in valle, dimidiaeque Galaad, usque ad torrentem Ieboc, qui est terminus filiorum Ammon.
Sihoni, mfalme wa Waamori, aliishi katika Heshiboni. Alitawala kutoka Aroeri, ambayo iko juu ya bonde la Arnoni kutoka katikati ya bonde, na nusu ya Geleadi kushuka mpaka Mto Yaboki katika mpaka wa Waamori.
3 et a solitudine usque ad Mare Ceneroth contra Orientem, et usque ad Mare deserti, quod est mare salsissimum, ad Orientalem plagam per viam quae ducit Bethsimoth: et ab australi parte, quae subiacet Asedoth, Phasga.
Sihoni pia alitawala juu ya Araba mpaka Bahari ya Kinerethi, kwenda mashariki, kuelekea Bahari ya Araba (Bahari ya Chumvi) upande wa mashariki, hadi huko Bethi Yeshimothi na upande wa kusini, kuelekea chini ya miteremko wa Mlima Pisiga.
4 Terminus Og regis Basan, de reliquiis Raphaim, qui habitavit in Astaroth, et in Edrai, et dominatus est in monte Hermon, et in Salecha, atque in universa Basan, usque ad terminos
Ogu, mfalme wa Bashani, mmoja kati ya mabaki ya Rephaimu, aliyeishi huko Shatarothi na Edrei.
5 Gessuri, et Machati, et dimidiae partis Galaad: terminos Sehon regis Hesebon.
Alitawala juu ya Mlima Hermoni, Saleka, na Bahani yote, hadi mpaka wa watu wa Geshuri na Wamakathi, na nusu ya Gleadi, hadi kufika mpaka wa Sihohi, mfalme wa Heshboni.
6 Moyses famulus Domini, et filii Israel percusserunt eos, tradiditque Terram eorum Moyses in possessionem Rubenitis, et Gaditis, et dimidiae tribui Manasse.
Musa mtumishi wa Yahweh, na watu wa Israeli walikuwa wamewashinda, na Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa nchi kama mali ya Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.
7 Hi sunt reges Terrae, quos percussit Iosue et filii Israel trans Iordanem ad Occidentalem plagam, a Baalgad in campo Libani, usque ad montem, cuius pars ascendit in Seir: tradiditque eam Iosue in possessionem tribubus Israel, singulis partes suas,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambayo Yoshua na watu wa Israeli waliwashinda katika upande wa magharibi mwa mto Yordani, kutoka Baali Gadi katika bonde karibu na Lebanoni hadi Mlima Halaki karibu na Edom. Yoshua aliyapa nchi makabila ya Israeli ili yaimiliki.
8 tam in montanis quam in planis atque campestribus. In Aseroth, et in solitudine, ac in meridie Hethaeus fuit et Amorrhaeus, Chananaeus et Pherezaeus, Hevaeus et Iebusaeus.
Aliwapa nchi ya milima, tambarare, Araba, sehemu za milima, nyika na Negevu, nchi ya Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
9 Rex Iericho unus: rex Hai, quae est ex latere Bethel, unus:
Wafalme hawa walikuwa ni mfalme wa Yeriko, mfalme wa Ai iliyo karibu na Betheli,
10 rex Ierusalem unus, rex Hebron unus,
mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Enaimu,
11 rex Ierimoth unus, rex Lachis unus,
mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi,
12 rex Eglon unus, rex Gazer unus,
mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,
13 rex Dabir unus, rex Gader unus,
mfalme wa Debiri, mfalme wa Gederi,
14 rex Herma unus, rex Hered unus,
mfalme wa Horima, mfalme wa Aradi,
15 rex Lebna unus, rex Adullam unus,
mfalme wa Libna, mfalme wa Adula,
16 rex Maceda unus, rex Bethel unus,
mfalme wa Makeda, mfalme wa Betheli,
17 rex Taphua unus, rex Opher unus,
mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi,
18 rex Aphec unus, rex Saron unus,
mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni,
19 rex Madon unus, rex Asor unus,
mfalme wa Madoni, mfalme wa Hazori,
20 rex Semeron unus, rex Achsaph unus,
mfalme wa Shimroni - Meroni, mfalme wa Akshafu.
21 rex Thenac unus, rex Mageddo unus,
mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido,
22 rex Cades unus, rex Iachanan Carmeli unus,
mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Jokineamu katika Karmeli,
23 rex Dor, et provinciae Dor unus, rex Gentium Galgal unus,
mfalme wa Dori katika Nafutali Dori, mfalme Goyimu katika Giligali, na
24 rex Thersa unus: omnes reges triginta unus.
mfalme Tiriza. Hesabu ya wafalme ilikuwa ni thelathini na moja kwa ujumla wake.