< Iosue 12 >

1 Hi sunt reges, quos percusserunt filii Israel, et possederunt Terram eorum trans Iordanem ad solis ortum, a torrente Arnon usque ad montem Hermon, et omnem Orientalem plagam, quae respicit solitudinem.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Sehon rex Amorrhaeorum, qui habitavit in Hesebon, dominatus est ab Aroer, quae sita est super ripam torrentis Arnon, et mediae partis in valle, dimidiaeque Galaad, usque ad torrentem Ieboc, qui est terminus filiorum Ammon.
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 et a solitudine usque ad Mare Ceneroth contra Orientem, et usque ad Mare deserti, quod est mare salsissimum, ad Orientalem plagam per viam quae ducit Bethsimoth: et ab australi parte, quae subiacet Asedoth, Phasga.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 Terminus Og regis Basan, de reliquiis Raphaim, qui habitavit in Astaroth, et in Edrai, et dominatus est in monte Hermon, et in Salecha, atque in universa Basan, usque ad terminos
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 Gessuri, et Machati, et dimidiae partis Galaad: terminos Sehon regis Hesebon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moyses famulus Domini, et filii Israel percusserunt eos, tradiditque Terram eorum Moyses in possessionem Rubenitis, et Gaditis, et dimidiae tribui Manasse.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 Hi sunt reges Terrae, quos percussit Iosue et filii Israel trans Iordanem ad Occidentalem plagam, a Baalgad in campo Libani, usque ad montem, cuius pars ascendit in Seir: tradiditque eam Iosue in possessionem tribubus Israel, singulis partes suas,
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 tam in montanis quam in planis atque campestribus. In Aseroth, et in solitudine, ac in meridie Hethaeus fuit et Amorrhaeus, Chananaeus et Pherezaeus, Hevaeus et Iebusaeus.
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 Rex Iericho unus: rex Hai, quae est ex latere Bethel, unus:
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 rex Ierusalem unus, rex Hebron unus,
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 rex Ierimoth unus, rex Lachis unus,
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 rex Eglon unus, rex Gazer unus,
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 rex Dabir unus, rex Gader unus,
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 rex Herma unus, rex Hered unus,
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 rex Lebna unus, rex Adullam unus,
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 rex Maceda unus, rex Bethel unus,
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 rex Taphua unus, rex Opher unus,
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 rex Aphec unus, rex Saron unus,
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 rex Madon unus, rex Asor unus,
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 rex Semeron unus, rex Achsaph unus,
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 rex Thenac unus, rex Mageddo unus,
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 rex Cades unus, rex Iachanan Carmeli unus,
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 rex Dor, et provinciae Dor unus, rex Gentium Galgal unus,
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 rex Thersa unus: omnes reges triginta unus.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Iosue 12 >