< Jonas Propheta 2 >

1 Et oravit Ionas ad Dominum Deum suum de ventre piscis.
Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake.
2 Et dixit: Clamavi de tribulatione mea ad Dominum, et exaudivit me: de ventre inferi clamavi, et exaudisti vocem meam. (Sheol h7585)
Akasema: “Katika shida yangu nalimwita Bwana, naye akanijibu. Kutoka kina cha kaburi niliomba msaada, nawe ukasikiliza kilio changu. (Sheol h7585)
3 Et proiecisti me in profundum in corde maris, et flumen circumdedit me: omnes gurgites tui, et fluctus tui super me transierunt.
Ulinitupa kwenye kilindi, ndani kabisa ya moyo wa bahari, mikondo ya maji ilinizunguka, mawimbi yako yote na viwimbi vilipita juu yangu.
4 Et ego dixi: Abiectus sum a conspectu oculorum tuorum: verumtamen rursus videbo templum sanctum tuum.
Nikasema, ‘Nimefukuziwa mbali na uso wako, hata hivyo nitatazama tena kuelekea Hekalu lako takatifu.’
5 Circumdederunt me aquae usque ad animam: abyssus vallavit me, pelagus operuit caput meum.
Maji yaliyonimeza yalinitisha, kilindi kilinizunguka; mwani ulijisokota kichwani pangu.
6 Ad extrema montium descendi: terrae vectes concluserunt me in aeternum: et sublevabis de corruptione vitam meam, Domine Deus meus.
Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima, makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele. Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni, Ee Bwana Mungu wangu.
7 Cum angustiaretur in me anima mea, Domini recordatus sum: ut veniat ad te oratio mea ad templum sanctum tuum.
“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka, nilikukumbuka wewe, Bwana, nayo maombi yangu yalikufikia wewe, katika Hekalu lako takatifu.
8 Qui custodiunt vanitates frustra, misericordiam suam derelinquunt.
“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.
9 Ego autem in voce laudis immolabo tibi: quaecumque vovi, reddam pro salute Domino.
Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea dhabihu. Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza. Wokovu watoka kwa Bwana.”
10 Et dixit Dominus pisci: et evomuit Ionam in aridam.
Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

< Jonas Propheta 2 >