< Job 9 >

1 Et respondens Iob, ait:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Vere scio quod ita sit, et quod non iustificetur homo compositus Deo.
“kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
3 Si voluerit contendere cum eo, non poterit ei respondere unum pro mille.
Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
4 Sapiens corde est, et fortis robore: quis restitit ei, et pacem habuit?
Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
5 Qui transtulit montes, et nescierunt hi quos subvertit in furore suo.
ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
6 Qui commovet terram de loco suo, et columnae eius concutiuntur.
ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
7 Qui praecipit Soli, et non oritur: et stellas claudit quasi sub signaculo:
Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
8 Qui extendit caelos solus, et graditur super fluctus maris.
ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
9 Qui facit Arcturum, et Oriona, et Hyadas, et interiora austri.
ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
10 Qui facit magna, et incomprehensibilia, et mirabilia, quorum non est numerus.
Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
11 Si venerit ad me, non videbo eum: si abierit, non intelligam.
Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
12 Si repente interroget, quis respondebit ei? vel quis dicere potest: Cur ita facis?
Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
13 Deus, cuius irae nemo resistere potest, et sub quo curvantur qui portant orbem.
Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
14 Quantus ergo sum ego, ut respondeam ei, et loquar verbis meis cum eo?
Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
15 Qui etiam si habuero quippiam iustum, non respondebo, sed meum iudicem deprecabor.
Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
16 Et cum invocantem exaudierit me, non credo quod audierit vocem meam.
Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
17 In turbine enim conteret me, et multiplicabit vulnera mea etiam sine causa.
kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
18 Non concedit requiescere spiritum meum, et implet me amaritudinibus.
Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
19 Si fortitudo quaeritur, robustissimus est: si aequitas iudicii, nemo audet pro me testimonium dicere.
Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
20 Si iustificare me voluero, os meum condemnabit me: si innocentem ostendero, pravum me comprobabit.
Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
21 Etiam si simplex fuero, hoc ipsum ignorabit anima mea, et taedebit me vitae meae.
Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
22 Unum est quod locutus sum, et innocentem et impium ipse consumit.
Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
23 Si flagellat, occidat semel, et non de poenis innocentum rideat.
Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
24 Terra data est in manus impii, vultum iudicum eius operit: quod si non ille est, quis ergo est?
Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
25 Dies mei velociores fuerunt cursore: fugerunt, et non viderunt bonum.
Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
26 Pertransierunt quasi naves poma portantes, sicut aquila volans ad escam.
Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
27 Cum dixero: Nequaquam ita loquar: commuto faciem meam, et dolore torqueor.
Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
28 Verebar omnia opera mea, sciens quod non parceres delinquenti.
Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
29 Si autem et sic impius sum, quare frustra laboravi?
Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
30 Si lotus fuero quasi aquis nivis, et fulserint velut mundissimae manus meae:
Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
31 Tamen sordibus intinges me, et abominabuntur me vestimenta mea.
Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
32 Neque enim viro qui similis mei est, respondebo: nec qui mecum in iudicio ex aequo possit audiri.
Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
33 Non est qui utrumque valeat arguere, et ponere manum suam in ambobus.
Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
34 Auferat a me virgam suam, et pavor eius non me terreat.
Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
35 Loquar, et non timebo eum: neque enim possum metuens respondere.
Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.

< Job 9 >