< Job 6 >

1 Respondens autem Iob, dixit:
Kisha Ayubu akajibu:
2 Utinam appenderentur peccata mea, quibus iram merui: et calamitas, quam patior, in statera.
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Quasi arena maris haec gravior appareret: unde et verba mea dolore sunt plena:
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Quia sagittae Domini in me sunt, quarum indignatio ebibit spiritum meum, et terrores Domini militant contra me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Numquid rugiet onager cum habuerit herbam? aut mugiet bos cum ante praesepe plenum steterit?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Aut poterit comedi insulsum, quod non est sale conditum? aut potest aliquis gustare, quod gustatum affert mortem?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Quae prius nolebat tangere anima mea, nunc prae angustia, cibi mei sunt.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Quis det ut veniat petitio mea: et quod expecto, tribuat mihi Deus?
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 Et qui coepit, ipse me conterat: solvat manum suam, et succidat me?
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Et haec mihi sit consolatio ut affligens me dolore, non parcat, nec contradicam sermonibus Sancti.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 Quae est enim fortitudo mea ut sustineam? aut quis finis meus, ut patienter agam?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Nec fortitudo lapidum fortitudo mea, nec caro mea aenea est.
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Ecce, non est auxilium mihi in me, et necessarii quoque mei recesserunt a me.
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 Qui tollit ab amico suo misericordiam, timorem Domini derelinquit.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Fratres mei praeterierunt me, sicut torrens qui raptim transit in convallibus.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Qui timent pruinam, irruet super eos nix.
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 Tempore, quo fuerint dissipati, peribunt: et ut incaluerint, solventur de loco suo.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Involutae sunt semitae gressuum eorum: ambulabunt in vacuum, et peribunt.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Considerate semitas Thema, itinera Saba, et expectate paulisper.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 Confusi sunt, quia speravi: venerunt quoque usque ad me, et pudore cooperti sunt.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Nunc venistis: et modo videntes plagam meam timetis.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Numquid dixi: Afferte mihi, et de substantia vestra donate mihi?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 Vel, Liberate me de manu hostis, et de manu robustorum eruite me?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Docete me, et ego tacebo: et siquid forte ignoravi, instruite me.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Quare detraxistis sermonibus veritatis, cum e vobis nullus sit qui possit arguere me?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Ad increpandum tantum eloquia concinnatis, et in ventum verba profertis.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Super pupillum irruitis, et subvertere nitimini amicum vestrum.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Verumtamen quod coepistis explete: praebete aurem, et videte an mentiar.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Respondete obsecro absque contentione: et loquentes id quod iustum est, iudicate.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Et non invenietis in lingua mea iniquitatem, nec in faucibus meis stultitia personabit.
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >