< Job 5 >

1 Voca ergo, si est qui tibi respondeat, et ad aliquem sanctorum convertere.
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Vere stultum interficit iracundia, et parvulum occidit invidia.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Ego vidi stultum firma radice, et maledixi pulchritudini eius statim.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Longe fient filii eius a salute, et conterentur in porta, et non erit qui eruat.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Cuius messem famelicus comedet, et ipsum rapiet armatus, et bibent sitientes divitias eius.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Nihil in terra sine causa fit, et de humo non oritur dolor.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Homo nascitur ad laborem, et avis ad volatum.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Quam ob rem ego deprecabor Dominum, et ad Deum ponam eloquium meum:
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 Qui facit magna et inscrutabilia et mirabilia absque numero:
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Qui dat pluviam super faciem terrae, et irrigat aquis universa:
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Qui ponit humiles in sublime, et moerentes erigit sospitate:
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 Qui dissipat cogitationes malignorum, ne possint implere manus eorum quod coeperant:
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Qui apprehendit sapientes in astutia eorum, et consilium pravorum dissipat:
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 Per diem incurrent tenebras, et quasi in nocte sic palpabunt in meridie.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Porro salvum faciet egenum a gladio oris eorum, et de manu violenti pauperem.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Et erit egeno spes, iniquitas autem contrahet os suum.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Beatus homo qui corripitur a Deo: increpationem ergo Domini ne reprobes:
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Quia ipse vulnerat, et medetur: percutit, et manus eius sanabunt.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 In sex tribulationibus liberabit te, et in septima non tangent te malum.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 In fame eruet te de morte, et in bello de manu gladii.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 A flagello linguae absconderis, et non timebis calamitatem cum venerit.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 In vastitate, et fame ridebis, et bestias terrae non formidabis.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Sed cum lapidibus regionum pactum tuum, et bestiae terrae pacificae erunt tibi.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 Et scies quod pacem habeat tabernaculum tuum, et visitans speciem tuam, non peccabis.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Scies quoque quoniam multiplex erit semen tuum, et progenies tua quasi herba terrae.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Ingredieris in abundantia sepulchrum, sicut infertur acervus tritici in tempore suo.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Ecce, hoc, ut investigavimus, ita est: quod auditum, mente pertracta.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >