< Job 40 >

1 Et adiecit Dominus, et locutus est ad Iob:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Numquid qui contendit cum Deo, tam facile conquiescit? utique qui arguit Deum, debet respondere ei.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Respondens autem Iob Domino, dixit:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Qui leviter locutus sum, respondere quid possum? manum meam ponam super os meum.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Unum locutus sum, quod utinam non dixissem: et alterum, quibus ultra non addam.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Respondens autem Dominus Iob de turbine, dixit:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Accinge sicut vir lumbos tuos: interrogabo te: et indica mihi.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Numquid irritum facies iudicium meum: et condemnabis me, ut tu iustificeris?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Et si habes brachium sicut Deus, et si voce simili tonas?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Circumda tibi decorem, et in sublime erigere, et esto gloriosus, et speciosis induere vestibus.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Disperge superbos in furore tuo, et respiciens omnem arrogantem humilia.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Respice cunctos superbos, et confunde eos, et contere impios in loco suo.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Absconde eos in pulvere simul, et facies eorum demerge in foveam:
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Et ego confitebor quod salvare te possit dextera tua.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Ecce, Behemoth, quem feci tecum, foenum quasi bos comedet:
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Fortitudo eius in lumbis eius, et virtus illius in umbilico ventris eius.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Stringit caudam suam quasi cedrum, nervi testiculorum eius perplexi sunt.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Ossa eius velut fistulae aeris, cartilago illius quasi laminae ferreae.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Ipse est principium viarum Dei, qui fecit eum, applicabit gladium eius.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Huic montes herbas ferunt: omnes bestiae agri ludent ibi.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Sub umbra dormit in secreto calami, et in locis humentibus.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Protegunt umbrae umbram eius, circumdabunt eum salices torrentis.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Ecce, absorbebit fluvium, et non mirabitur: et habet fiduciam quod influat Iordanis in os eius.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 In oculis eius quasi hamo capiet eum, et in sudibus perforabit nares eius.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >