< Job 38 >
1 Respondens autem Dominus Iob de turbine, dixit:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Quis est iste involvens sententias sermonibus imperitis?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Accinge sicut vir lumbos tuos: interrogabo te, et responde mihi.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Ubi eras quando ponebam fundamenta terrae? indica mihi si habes intelligentiam.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Quis posuit mensuras eius, si nosti? vel quis tetendit super eam lineam?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Super quo bases illius solidatae sunt? aut quis demisit lapidem angularem eius,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Cum me laudarent simul astra matutina, et iubilarent omnes filii Dei?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Quis conclusit ostiis mare, quando erumpebat quasi de vulva procedens:
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 Cum ponerem nubem vestimentum eius, et caligine illud quasi pannis infantiae obvolverem?
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Circumdedi illud terminis meis, et posui vectem, et ostia:
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 Et dixi: Usque huc venies, et non procedes amplius, et hic confringes tumentes fluctus tuos.
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Numquid post ortum tuum praecepisti diluculo, et ostendisti aurorae locum suum?
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Et tenuisti concutiens extrema terrae, et excussisti impios ex ea?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Restituetur ut lutum signaculum, et stabit sicut vestimentum:
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Auferetur ab impiis lux sua, et brachium excelsum confringetur.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Numquid ingressus es profunda maris, et in novissimis abyssi deambulasti?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Numquid apertae sunt tibi portae mortis, et ostia tenebrosa vidisti?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Numquid considerasti latitudinem terrae? indica mihi, si nosti, omnia,
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 In qua via lux habitet, et tenebrarum quis locus sit:
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 Ut ducas unumquodque ad terminos suos, et intelligas semitas domus eius.
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Sciebas tunc quod nasciturus esses? et numerum dierum tuorum noveras?
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Numquid ingressus es thesauros nivis, aut thesauros grandinis aspexisti,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Quae praeparavi in tempus hostis, in diem pugnae et belli?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Per quam viam spargitur lux, dividitur aestus super terram?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Quis dedit vehementissimo imbri cursum, et viam sonantis tonitrui,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Ut plueret super terram absque homine in deserto, ubi nullus mortalium commoratur,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 Ut impleret inviam et desolatam, et produceret herbas virentes?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Quis est pluviae pater? vel quis genuit stillas roris?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 De cuius utero egressa est glacies? et gelu de caelo quis genuit?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 In similitudinem lapidis aquae durantur, et superficies abyssi constringitur.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Numquid coniungere valebis micantes stellas Pleiadas, aut gyrum Arcturi poteris dissipare?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Numquid producis Luciferum in tempore suo, et Vesperum super filios terrae consurgere facis?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Numquid nosti ordinem caeli, et pones rationem eius in terra?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Numquid elevabis in nebula vocem tuam, et impetus aquarum operiet te?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Numquid mittes fulgura, et ibunt, et revertentia dicent tibi: Adsumus?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Quis posuit in visceribus hominis sapientiam? vel quis dedit gallo intelligentiam?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Quis enarrabit caelorum rationem, et concentum caeli quis dormire faciet?
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 Quando fundebatur pulvis in terra, et glebae compingebantur?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Numquid capies leaenae praedam, et animam catulorum eius implebis,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 Quando cubant in antris, et in specubus insidiantur?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Quis praeparat corvo escam suam, quando pulli eius clamant ad eum, vagientes, eo quod non habeant cibos?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?