< Job 36 >

1 Addens quoque Eliu, haec locutus est:
Elihu akaendelea kusema:
2 Sustine me paululum, et indicabo tibi: adhuc enim habeo quod pro Deo loquar.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 Repetam scientiam meam a principio, et operatorem meum probabo iustum.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 Vere enim absque mendacio sermones mei, et perfecta scientia probabitur tibi.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Deus potentes non abiicit, cum et ipse sit potens.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 Sed non salvat impios, et iudicium pauperibus tribuit.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 Non auferet a iusto oculos suos, et reges in solio collocat in perpetuum, et illic eriguntur.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 Et si fuerint in catenis, et vinciantur funibus paupertatis.
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Indicabit eis opera eorum, et scelera eorum, quia violenti fuerunt.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 Revelabit quoque aurem eorum, ut corripiat: et loquetur, ut revertantur ab iniquitate.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 Si audierint et observaverint, complebunt dies suos in bono, et annos suos in gloria:
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 Si autem non audierint, transibunt per gladium, et consumentur in stultitia.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 Simulatores et callidi provocant iram Dei, neque clamabunt cum vincti fuerint.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 Morietur in tempestate anima eorum, et vita eorum inter effeminatos.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 Eripiet de angustia sua pauperem, et revelabit in tribulatione aurem eius.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Igitur salvabit te de ore angusto latissime, et non habente fundamentum subter se: requies autem mensae tuae erit plena pinguedine.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 Causa tua quasi impii iudicata est, causam iudiciumque recipies.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Non te ergo superet ira, ut aliquem opprimas: nec multitudo donorum inclinet te.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Depone magnitudinem tuam absque tribulatione, et omnes robustos fortitudine.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Ne protrahas noctem, ut ascendant populi pro eis.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Cave ne declines ad iniquitatem: hanc enim coepisti sequi post miseriam.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Ecce, Deus excelsus in fortitudine sua, et nullus ei similis in legislatoribus.
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Quis poterit scrutari vias eius? aut quis potest ei dicere: Operatus es iniquitatem?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Memento quod ignores opus eius, de quo cecinerunt viri.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Omnes homines vident eum, unusquisque intuetur procul.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Ecce, Deus magnus vincens scientiam nostram: numerus annorum eius inaestimabilis.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 Qui aufert stillas pluviae, et effundit imbres ad instar gurgitum.
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Qui de nubibus fluunt, quae praetexunt cuncta desuper.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Si voluerit extendere nubes quasi tentorium suum.
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Et fulgurare lumine suo desuper, cardines quoque maris operiet.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 Per haec enim iudicat populos, et dat escas multis mortalibus.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 In manibus abscondit lucem, et praecepit ei ut rursus adveniat.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Annunciat de ea amico suo, quod possessio eius sit, ut ad eam possit ascendere.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >