< Job 35 >

1 Igitur Eliu haec rursum locutus est:
Aidha, Elihu aliendelea kusema,
2 Numquid aequa tibi videtur tua cogitatio, ut diceres: Iustior sum Deo?
“Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
3 Dixisti enim: Non tibi placet quod rectum est: vel quid tibi proderit, si ego peccavero?
Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
4 Itaque ego respondebo sermonibus tuis, et amicis tuis tecum.
Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
5 Suspice caelum et intuere, et contemplare aethera quod altior te sit.
Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
6 Si peccaveris, quid ei nocebis? et si multiplicatae fuerint iniquitates tuae, quid facies contra eum?
Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
7 Porro si iuste egeris, quid donabis ei, aut quid de manu tua accipiet?
Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
8 Homini, qui similis tui est, nocebit impietas tua: et filium hominis adiuvabit iustitia tua.
Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
9 Propter multitudinem calumniatorum clamabunt: et eiulabunt propter vim brachii tyrannorum.
Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
10 Et non dixit: Ubi est Deus, qui fecit me, qui dedit carmina in nocte,
Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
11 Qui docet nos super iumenta terrae, et super volucres caeli erudit nos.
ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
12 Ibi clamabunt, et non exaudiet, propter superbiam malorum.
Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
13 Non ergo frustra audiet Deus, et Omnipotens causas singulorum intuebitur.
Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
14 Etiam cum dixeris: Non considerat: iudicare coram illo, et expecta eum.
Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
15 Nunc enim non infert furorem suum, nec ulciscitur scelus valde.
Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
16 Ergo Iob frustra aperit os suum, et absque scientia verba multiplicat.
Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”

< Job 35 >