< Job 34 >

1 Pronuncians itaque Eliu, etiam haec locutus est:
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 Audite sapientes verba mea, et eruditi auscultate me:
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 Auris enim verba probat, et guttur escas gustu diiudicat.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 Iudicium eligamus nobis, et inter nos videamus quid sit melius.
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 Quia dixit Iob: Iustus sum, et Deus subvertit iudicium meum.
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 In iudicando enim me, mendacium est: violenta sagitta mea absque ullo peccato.
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 Quis est vir ut est Iob, qui bibit subsannationem quasi aquam:
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 Qui graditur cum operantibus iniquitatem, et ambulat cum viris impiis?
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 Dixit enim: Non placebit vir Deo, etiam si cucurrerit cum eo.
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 Ideo viri cordati audite me, absit a Deo impietas, et ab Omnipotente iniquitas.
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 Opus enim hominis reddet ei, et iuxta vias singulorum restituet eis.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 Vere enim Deus non condemnabit frustra, nec Omnipotens subvertet iudicium.
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 Quem constituit alium super terram? aut quem posuit super orbem, quem fabricatus est?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 Si direxerit ad eum cor suum, spiritum illius et flatum ad se trahet.
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 Deficiet omnis caro simul, et homo in cinerem revertetur.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 Si habes ergo intellectum, audi quod dicitur, et ausculta vocem eloquii mei.
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 Numquid qui non amat iudicium, sanari potest? et quomodo tu eum, qui iustus est, in tantum condemnas?
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 Qui dicit regi, apostata: qui vocat duces impios:
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 Qui non accipit personas principum: nec cognovit tyrannum, cum disceptaret contra pauperem: opus enim manuum eius sunt universi.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 Subito morientur, et in media nocte turbabuntur populi, et pertransibunt, et auferent violentum absque manu.
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 Oculi enim eius super vias hominum, et omnes gressus eorum considerat.
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 Non sunt tenebrae, et non est umbra mortis, ut abscondantur ibi qui operantur iniquitatem.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 Neque enim ultra in hominis potestate est, ut veniat ad Deum in iudicium.
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 Conteret multos, et innumerabiles, et stare faciet alios pro eis.
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Novit enim opera eorum: et idcirco inducet noctem, et conterentur.
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 Quasi impios percussit eos in loco videntium.
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 Qui quasi de industria recesserunt ab eo, et omnes vias eius intelligere noluerunt:
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 Ut pervenire facerent ad eum clamorem egeni, et audiret vocem pauperum.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 Ipso enim concedente pacem, quis est qui condemnet? ex quo absconderit vultum, quis est qui contempletur eum et super gentes et super omnes homines?
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 Qui regnare facit hominem hypocritam propter peccata populi.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 Quia ergo ego locutus sum ad Deum, te quoque non prohibebo.
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 Si erravi, tu doce me: si iniquitatem locutus sum, ultra non addam.
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 Numquid a te Deus expetit eam, quia displicuit tibi? tu enim coepisti loqui, et non ego: quod si quid nosti melius, loquere.
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Viri intelligentes loquantur mihi, et vir sapiens audiat me.
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 Iob autem stulte locutus est, et verba illius non sonant disciplinam.
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 Pater mi, probetur Iob usque ad finem: ne desinas ab homine iniquitatis.
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 Qui addit super peccata sua blasphemiam, inter nos interim constringatur: et tunc ad iudicium provocet sermonibus suis Deum.
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”

< Job 34 >