< Job 34 >

1 Pronuncians itaque Eliu, etiam haec locutus est:
Kisha Elihu akasema:
2 Audite sapientes verba mea, et eruditi auscultate me:
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
3 Auris enim verba probat, et guttur escas gustu diiudicat.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
4 Iudicium eligamus nobis, et inter nos videamus quid sit melius.
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
5 Quia dixit Iob: Iustus sum, et Deus subvertit iudicium meum.
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
6 In iudicando enim me, mendacium est: violenta sagitta mea absque ullo peccato.
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
7 Quis est vir ut est Iob, qui bibit subsannationem quasi aquam:
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
8 Qui graditur cum operantibus iniquitatem, et ambulat cum viris impiis?
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
9 Dixit enim: Non placebit vir Deo, etiam si cucurrerit cum eo.
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
10 Ideo viri cordati audite me, absit a Deo impietas, et ab Omnipotente iniquitas.
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11 Opus enim hominis reddet ei, et iuxta vias singulorum restituet eis.
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12 Vere enim Deus non condemnabit frustra, nec Omnipotens subvertet iudicium.
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13 Quem constituit alium super terram? aut quem posuit super orbem, quem fabricatus est?
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14 Si direxerit ad eum cor suum, spiritum illius et flatum ad se trahet.
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15 Deficiet omnis caro simul, et homo in cinerem revertetur.
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
16 Si habes ergo intellectum, audi quod dicitur, et ausculta vocem eloquii mei.
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
17 Numquid qui non amat iudicium, sanari potest? et quomodo tu eum, qui iustus est, in tantum condemnas?
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
18 Qui dicit regi, apostata: qui vocat duces impios:
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
19 Qui non accipit personas principum: nec cognovit tyrannum, cum disceptaret contra pauperem: opus enim manuum eius sunt universi.
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
20 Subito morientur, et in media nocte turbabuntur populi, et pertransibunt, et auferent violentum absque manu.
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
21 Oculi enim eius super vias hominum, et omnes gressus eorum considerat.
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
22 Non sunt tenebrae, et non est umbra mortis, ut abscondantur ibi qui operantur iniquitatem.
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
23 Neque enim ultra in hominis potestate est, ut veniat ad Deum in iudicium.
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
24 Conteret multos, et innumerabiles, et stare faciet alios pro eis.
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
25 Novit enim opera eorum: et idcirco inducet noctem, et conterentur.
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
26 Quasi impios percussit eos in loco videntium.
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
27 Qui quasi de industria recesserunt ab eo, et omnes vias eius intelligere noluerunt:
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
28 Ut pervenire facerent ad eum clamorem egeni, et audiret vocem pauperum.
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
29 Ipso enim concedente pacem, quis est qui condemnet? ex quo absconderit vultum, quis est qui contempletur eum et super gentes et super omnes homines?
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
30 Qui regnare facit hominem hypocritam propter peccata populi.
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
31 Quia ergo ego locutus sum ad Deum, te quoque non prohibebo.
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
32 Si erravi, tu doce me: si iniquitatem locutus sum, ultra non addam.
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
33 Numquid a te Deus expetit eam, quia displicuit tibi? tu enim coepisti loqui, et non ego: quod si quid nosti melius, loquere.
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
34 Viri intelligentes loquantur mihi, et vir sapiens audiat me.
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
35 Iob autem stulte locutus est, et verba illius non sonant disciplinam.
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
36 Pater mi, probetur Iob usque ad finem: ne desinas ab homine iniquitatis.
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
37 Qui addit super peccata sua blasphemiam, inter nos interim constringatur: et tunc ad iudicium provocet sermonibus suis Deum.
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

< Job 34 >