< Job 33 >
1 Audi igitur Iob eloquia mea, et omnes sermones meos ausculta.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Ecce aperui os meum, loquatur lingua mea in faucibus meis.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Simplici corde meo sermones mei, et sententiam puram labia mea loquentur.
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 Spiritus Dei fecit me, et spiraculum Omnipotentis vivificavit me.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Si potes, responde mihi, et adversus faciem meam consiste.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Ecce, et me sicut et te fecit Deus, et de eodem luto ego quoque formatus sum.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Verumtamen miraculum meum non te terreat, et eloquentia mea non sit tibi gravis.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 Dixisti ergo in auribus meis, et vocem verborum tuorum audivi:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 Mundus sum ego, et absque delicto: immaculatus, et non est iniquitas in me.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Quia querelas in me reperit, ideo arbitratus est me inimicum sibi.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Posuit in nervo pedes meos, custodivit omnes semitas meas.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Hoc est ergo, in quo non es iustificatus: respondebo tibi, quia maior sit Deus homine.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 Adversus eum contendis quod non ad omnia verba responderit tibi?
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Semel loquitur Deus, et secundo idipsum non repetit.
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 Per somnium in visione nocturna, quando irruit sopor super homines, et dormiunt in lectulo:
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Tunc aperit aures virorum, et erudiens eos instruit disciplina,
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 Ut avertat hominem ab his, quae facit, et liberet eum de superbia:
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 Eruens animam eius a corruptione: et vitam illius, ut non transeat in gladium.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 Increpat quoque per dolorem in lectulo, et omnia ossa eius marcescere facit.
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 Abominabilis ei fit in vita sua panis, et animae illius cibus ante desiderabilis.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Tabescet caro eius, et ossa, quae tecta fuerant, nudabuntur.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Appropinquavit corruptioni anima eius, et vita illius mortiferis.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Si fuerit pro eo Angelus loquens, unus de millibus, ut annunciet hominis aequitatem:
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 Miserebitur eius, et dicet: Libera eum, ut non descendat in corruptionem: inveni in quo ei propitier.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 Consumpta est caro eius a suppliciis, revertatur ad dies adolescentiae suae.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Deprecabitur Deum, et placabilis ei erit: et videbit faciem eius in iubilo, et reddet homini iustitiam suam.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Respiciet homines, et dicet: Peccavi, et vere deliqui, et, ut eram dignus, non recepi.
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 Liberavit animam suam ne pergeret in interitum, sed vivens lucem videret.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 Ecce, haec omnia operatur Deus tribus vicibus per singulos.
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 Ut revocet animas eorum a corruptione, et illuminet luce viventium.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Attende Iob, et audi me: et tace, dum ego loquor.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Si autem habes quod loquaris, responde mihi, loquere: volo enim, te apparere iustum.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 Quod si non habes, audi me: tace, et docebo te sapientiam.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”