< Job 31 >

1 Pepigi foedus cum oculis meis ut ne cogitarem quidem de virgine.
“Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.
2 Quam enim partem haberet in me Deus desuper, et hereditatem Omnipotens de excelsis?
Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu, urithi wake kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu Aliye juu?
3 Numquid non perditio est iniquo, et alienatio operantibus iniustitiam?
Je, si uharibifu kwa watu waovu, maangamizi kwa wale watendao mabaya?
4 Nonne ipse considerat vias meas, et cunctos gressus meos dinumerat?
Je, yeye hazioni njia zangu na kuihesabu kila hatua yangu?
5 Si ambulavi in vanitate, et festinavit in dolo pes meus:
“Kama nimeishi katika uongo au mguu wangu umekimbilia udanganyifu,
6 Appendat me in statera iusta, et sciat Deus simplicitatem meam.
Mungu na anipime katika mizani za uaminifu, naye atajua kwamba sina hatia:
7 Si declinavit gressus meus de via, et si secutus est oculus meus cor meum, et si manibus meis adhaesit macula:
kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia, kama moyo wangu umeongozwa na macho yangu, au kama mikono yangu imetiwa unajisi,
8 Seram, et alius comedat: et progenies mea eradicetur.
basi wengine na wale nilichokipanda, nayo yale yote niliyootesha na yangʼolewe.
9 Si deceptum est cor meum super muliere, et si ad ostium amici mei insidiatus sum:
“Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke, au kama nimevizia mlangoni mwa jirani yangu,
10 Scortum alterius sit uxor mea, et super illam incurventur alii.
basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine, nao wanaume wengine walale naye.
11 Hoc enim nefas est, et iniquitas maxima.
Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu, naam, dhambi ya kuhukumiwa.
12 Ignis est usque ad perditionem devorans, et omnia eradicans genimina.
Ni moto uwakao kwa Uharibifu; ungekuwa umengʼoa mavuno yangu.
13 Si contempsi subire iudicium cum servo meo, et ancilla mea, cum disceptarent adversum me.
“Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu, walipokuwa na manungʼuniko dhidi yangu,
14 Quid enim faciam cum surrexerit ad iudicandum Deus? et cum quaesierit, quid respondebo illi?
nitafanya nini Mungu atakaponikabili? Nitamjibu nini nitakapoitwa kutoa hesabu?
15 Numquid non in utero fecit me qui et illum operatus est: et formavit me in vulva unus?
Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu, si ndiye aliwaumba? Je, si ni yeye huyo mmoja aliyetuumba sote ndani ya mama zetu?
16 Si negavi, quod volebant, pauperibus, et oculos viduae expectare feci:
“Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, au kuyaacha macho ya wajane yadhoofike,
17 Si comedi buccellam meam solus, et non comedit pupillus ex ea:
kama nimekula chakula changu mwenyewe, bila kuwashirikisha yatima;
18 (Quia ab infantia mea crevit mecum miseratio: et de utero matris meae egressa est mecum.)
lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya, nami tangu kuzaliwa kwangu nimewaongoza wajane:
19 Si despexi pereuntem, eo quod non habuerit indumentum, et absque operimento pauperem:
kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo, au mtu mhitaji asiye na mavazi
20 Si non benedixerunt mihi latera eius, et de velleribus ovium mearum calefactus est:
ambaye wala moyo wake haukunibariki kwa kumpatia joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo zangu,
21 Si levavi super pupillum manum meam, etiam cum viderem me in porta superiorem:
na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima, nikijua kuwa nina ushawishi mahakamani,
22 Humerus meus a iunctura sua cadat, et brachium meum cum suis ossibus confringatur.
basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu, nao na uvunjike kutoka kiungio chake.
23 Semper enim quasi tumentes super me fluctus timui Deum, et pondus eius ferre non potui.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu, nami kwa kuuogopa utukufu wake sikuweza kufanya mambo kama hayo.
24 Si putavi aurum robur meum, et obrizo dixi: Fiducia mea.
“Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu, au kuiambia dhahabu safi, ‘Wewe ndiwe salama yangu,’
25 Si laetatus sum super multis divitiis meis, et quia plurima reperit manus mea.
kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu, ustawi ambao mikono yangu ilikuwa imepata,
26 Si vidi solem cum fulgeret, et lunam incedentem clare:
kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake au mwezi ukienda kwa fahari yake,
27 Et laetatum est in abscondito cor meum, et osculatus sum manum meam ore meo.
hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri, au kubusu mkono wangu kwa kuviheshimu,
28 Quae est iniquitas maxima, et negatio contra Deum altissimum.
basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa, kwa kuwa ningekuwa si mwaminifu kwa Mungu aishiye juu sana.
29 Si gavisus sum ad ruinam eius, qui me oderat, et exultavi quod invenisset eum malum.
“Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu, au kutazama kwa furaha taabu iliyomjia,
30 Non enim dedi ad peccandum guttur meum, ut expeterem maledicens animam eius.
lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi kwa kuomba laana dhidi ya maisha yake;
31 Si non dixerunt viri tabernaculi mei: Quis det de carnibus eius ut saturemur?
kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema, ‘Ni nani ambaye hajashibishwa na nyama ya Ayubu?’
32 Foris non mansit peregrinus, ostium meum viatori patuit.
Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani, kwa maana mlango wangu ulikuwa wazi kwa msafiri;
33 Si abscondi quasi homo peccatum meum, et celavi in sinu meo iniquitatem meam.
kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo, kwa kuficha hatia yangu moyoni mwangu,
34 Si expavi ad multitudinem nimiam, et despectio propinquorum terruit me: et non magis tacui, nec egressus sum ostium.
kwa sababu ya kuogopa umati wa watu, na hivyo kuwa na hofu ya kudharauliwa na jamaa, nikanyamaza kimya nisitoke nje ya mlango:
35 Quis mihi tribuat auditorem, ut desiderium meum audiat Omnipotens: et librum scribat ipse qui iudicat.
(“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia! Tazama sasa ninatia sahihi kwenye utetezi wangu: Mwenyezi na anijibu; mshtaki wangu na aweke mashtaka yake kwenye maandishi.
36 Ut in humero meo portem illum, et circumdem illum quasi coronam mihi?
Hakika ningeyavaa begani mwangu, ningeyavaa kama taji.
37 Per singulos gradus meos pronunciabo illum, et quasi principi offeram eum.
Ningempa hesabu ya kila hatua yangu, ningemwendea kama mwana wa mfalme.)
38 Si adversum me terra mea clamat, et cum ipsa sulci eius deflent:
“Kama nchi yangu inalia dhidi yangu, na mifereji yake yote imelowana kwa machozi,
39 Si fructus eius comedi absque pecunia, et animam agricolarum eius afflixi:
kama nimekula mazao yake bila malipo, au kuvunja mioyo ya wapangaji wake,
40 Pro frumento oriatur mihi tribulus, et pro hordeo spina.
basi miiba na iote badala ya ngano, na magugu badala ya shayiri.” Mwisho wa maneno ya Ayubu.

< Job 31 >