< Job 29 >

1 Addidit quoque Iob, assumens parabolam suam, et dixit:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Quis mihi tribuat, ut sim iuxta menses pristinos secundum dies, quibus Deus custodiebat me?
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Quando splendebat lucerna eius super caput meum, et ad lumen eius ambulabam in tenebris?
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Sicut fui in diebus adolescentiae meae, quando secreto Deus erat in tabernaculo meo?
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Quando erat Omnipotens mecum: et in circuitu meo pueri mei?
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Quando lavabam pedes meos butyro, et petra fundebat mihi rivos olei?
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Quando procedebam ad portam civitatis, et in platea parabant cathedram mihi?
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Videbant me iuvenes, et abscondebantur: et senes assurgentes stabant.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Principes cessabant loqui, et digitum superponebant ori suo.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 Vocem suam cohibebant duces, et lingua eorum gutturi suo adhaerebat.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Auris audiens beatificabat me, et oculus videns testimonium reddebat mihi.
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Eo quod liberassem pauperem vociferantem, et pupillum, cui non esset adiutor.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 Benedictio perituri super me veniebat, et cor viduae consolatus sum.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 Iustitia indutus sum: et vestivi me, sicut vestimento et diademate, iudicio meo.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Oculus fui caeco, et pes claudo.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 Pater eram pauperum: et causam quam nesciebam, diligentissime investigabam.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 Conterebam molas iniqui, et de dentibus illius auferebam praedam.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Dicebamque: In nidulo meo moriar, et sicut palma multiplicabo dies.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Radix mea aperta est secus aquas, et ros morabitur in messione mea.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Gloria mea semper innovabitur, et arcus meus in manu mea instaurabitur.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 Qui me audiebant, expectabant sententiam, et intenti tacebant ad consilium meum.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Verbis meis addere nihil audebant, et super illos stillabat eloquium meum.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Expectabant me sicut pluviam, et os suum aperiebant quasi ad imbrem serotinum.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Siquando ridebam ad eos, non credebant, et lux vultus mei non cadebat in terram.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Si voluissem ire ad eos, sedebam primus: cumque sederem quasi rex, circumstante exercitu, eram tamen moerentium consolator.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.

< Job 29 >