< Job 28 >

1 Habet argentum, venarum suarum principia: et auro locus est, in quo conflatur.
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 Ferrum de terra tollitur: et lapis solutus calore, in aes vertitur.
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Tempus posuit tenebris, et universorum finem ipse considerat, lapidem quoque caliginis, et umbram mortis.
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 Dividit torrens a populo peregrinante, eos, quos oblitus est pes egentis hominis, et invios.
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 Terra, de qua oriebatur panis in loco suo, igni subversa est.
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 Locus sapphiri lapides eius, et glebae illius aurum.
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 Semitam ignoravit avis, nec intuitus est eam oculus vulturis.
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 Non calcaverunt eam filii institorum, nec pertransivit per eam leaena.
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 Ad silicem extendit manum suam, subvertit a radicibus montes.
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 In petris rivos excidit, et omne pretiosum vidit oculus eius.
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 Profunda quoque fluviorum scrutatus est, et abscondita in lucem produxit.
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 Sapientia vero ubi invenitur? et quis est locus intelligentiae?
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Nescit homo pretium eius, nec invenitur in terra suaviter viventium.
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 Abyssus dicit: Non est in me: et mare loquitur: Non est mecum.
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 Non dabitur aurum obrizum pro ea, nec appendetur argentum in commutatione eius.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 Non conferetur tinctis Indiae coloribus, nec lapidi sardonycho pretiosissimo, vel sapphiro.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Non adaequabitur ei aurum vel vitrum, nec commutabuntur pro ea vasa auri:
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 Excelsa et eminentia non memorabuntur comparatione eius: trahitur autem sapientia de occultis.
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 Non adaequabitur ei topazius de Aethiopia, nec tincturae mundissimae componetur.
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 Unde ergo sapientia venit? et quis est locus intelligentiae?
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 Abscondita est ab oculis omnium viventium, volucres quoque caeli latet.
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Perditio et mors dixerunt: Auribus nostris audivimus famam eius.
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 Deus intelligit viam eius, et ipse novit locum illius.
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 Ipse enim fines mundi intuetur: et omnia, quae sub caelo sunt, respicit.
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 Qui fecit ventis pondus, et aquas appendit in mensura.
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 Quando ponebat pluviis legem, et viam procellis sonantibus:
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 Tunc vidit illam, et enarravit, et praeparavit, et investigavit.
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 Et dixit homini: Ecce timor Domini, ipsa est sapientia: et recedere a malo, intelligentia.
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”

< Job 28 >