< Job 12 >

1 Respondens autem Iob, dixit:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 Ergo vos estis soli homines, et vobiscum morietur sapientia?
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Et mihi est cor sicut et vobis, nec inferior vestri sum: quis enim haec, quae nostis, ignorat?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Qui deridetur ab amico suo sicut ego, invocabit Deum, et exaudiet eum: deridetur enim iusti simplicitas.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Lampas contempta apud cogitationes divitum, parata ad tempus statutum.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Abundant tabernacula praedonum, et audacter provocant Deum, cum ipse dederit omnia in manus eorum.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Nimirum interroga iumenta, et docebunt te: et volatilia caeli, et indicabunt tibi.
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Loquere terrae, et respondebit tibi: et narrabunt pisces maris.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Quis ignorat quod omnia haec manus Domini fecerit?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 In cuius manu anima omnis viventis, et spiritus universae carnis hominis.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Nonne auris verba diiudicat, et fauces comedentis, saporem?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 In antiquis est sapientia, et in multo tempore prudentia.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Apud ipsum est sapientia et fortitudo, ipse habet consilium et intelligentiam.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Si destruxerit, nemo est qui aedificet: si incluserit hominem, nullus est qui aperiat.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Si continuerit aquas, omnia siccabuntur: et si emiserit eas, subvertent terram.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Apud ipsum est fortitudo et sapientia: ipse novit et decipientem, et eum qui decipitur.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Adducit consiliarios in stultum finem, et iudices in stuporem.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 Balteum regum dissolvit, et praecingit fune renes eorum.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 Ducit sacerdotes inglorios, et optimates supplantat:
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Commutans labium veracium, et doctrinam senum auferens.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Effundit despectionem super principes, eos, qui oppressi fuerant, relevans.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Qui revelat profunda de tenebris, et producit in lucem umbram mortis.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Qui multiplicat gentes et perdit eas, et subversas in integrum restituit.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Qui immutat cor principum populi terrae, et decipit eos ut frustra incedant per invium:
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Palpabunt quasi in tenebris, et non in luce, et errare eos faciet quasi ebrios.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >