< Job 10 >

1 Taedet animam meam vitae meae, dimittam adversum me eloquium meum, loquar in amaritudine animae meae.
“Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
2 Dicam Deo: Noli me condemnare: indica mihi cur me ita iudices.
Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
3 Numquid bonum tibi videtur, si calumnieris me, et opprimas me opus manuum tuarum, et consilium impiorum adiuves?
Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
4 Numquid oculi carnei tibi sunt: aut sicut videt homo, et tu videbis?
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
5 Numquid sicut dies hominis dies tui, et anni tui sicut humana sunt tempora,
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
6 Ut quaeras iniquitatem meam, et peccatum meum scruteris?
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
7 Et scias quia nihil impium fecerim, cum sit nemo qui de manu tua possit eruere.
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
8 Manus tuae fecerunt me, et plasmaverunt me totum in circuitu: et sic repente praecipitas me?
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
9 Memento quaeso quod sicut lutum feceris me, et in pulverem reduces me.
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
10 Nonne sicut lac mulsisti me, et sicut caseum me coagulasti?
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
11 Pelle et carnibus vestisti me: ossibus et nervis compegisti me.
ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
12 Vitam et misericordiam tribuisti mihi, et visitatio tua custodivit spiritum meum.
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
13 Licet haec celes in corde tuo, tamen scio quia universorum memineris.
“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
14 Si peccavi, et ad horam pepercisti mihi: cur ab iniquitate mea mundum me esse non pateris?
Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
15 Et si impius fuero, vae mihi est: et si iustus, non levabo caput, saturatus afflictione et miseria.
Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
16 Et propter superbiam quasi leaenam capies me, reversusque mirabiliter me crucias.
Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
17 Instauras testes tuos contra me, et multiplicas iram tuam adversum me, et poenae militant in me.
Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
18 Quare de vulva eduxisti me? qui utinam consumptus essem ne oculus me videret.
“Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
19 Fuissem quasi non essem, de utero translatus ad tumulum.
Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
20 Numquid non paucitas dierum meorum finietur brevi? dimitte ergo me, ut plangam paululum dolorem meum:
Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
21 Antequam vadam et non revertar, ad terram tenebrosam, et opertam mortis caligine:
kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
22 Terram miseriae et tenebrarum, ubi umbra mortis, et nullus ordo, sed sempiternus horror inhabitat.
nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”

< Job 10 >