< Genesis 10 >

1 Hae sunt generationes filiorum Noe, Sem, Cham, et Iapheth: natique sunt eis filii post diluvium.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Filii Iapheth: Gomer, et Magog, et Madai, et Iavan, et Thubal, et Mosoch, et Thiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Porro filii Gomer: Ascenez et Riphath et Thogorma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Filii autem Iavan: Elisa et Tharsis, Cetthim et Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Ab his divisae sunt insulae gentium in regionibus suis, unusquisque secundum linguam suam et familias suas in nationibus suis.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Filii autem Cham: Chus, et Mesraim, et Phuth, et Chanaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 Filii autem Chus: Saba, et Hevila, et Sabatha, et Regma, et Sabatacha. Filii Regma: Saba, et Dadan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Porro Chus genuit Nemrod: ipse coepit esse potens in terra,
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 et erat robustus venator coram Domino. Ob hoc exivit proverbium: Quasi Nemrod robustus venator coram Domino.
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Fuit autem principium regni eius Babylon, et Arach, et Achad, et Chalanne, in terra Sennaar.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 De terra illa egressus est Assur, et aedificavit Niniven, et plateas civitatis, et Chale.
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 Resen quoque inter Niniven et Chale: haec est civitas magna.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 At vero Mesraim genuit Ludim, et Anamim, et Laabim, et Nephthuim,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 et Phetrusim, et Chasluim: de quibus egressi sunt Philisthiim et Caphtorim.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Chanaan autem genuit Sidonem primogenitum suum, Hethaeum,
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 et Iebusaeum, et Amorrhaeum, et Gergesaeum,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 et Hevaeum, et Aracaeum: Sinaeum,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 et Aradium, Samaraeum et Amathaeum: et per hos disseminati sunt populi Chananaeorum.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 Factique sunt termini Chanaan venientibus a Sidone Geraram usque ad Gazam, donec ingrediaris Sodomam et Gomorrham, et Adamam, et Seboim usque Lasa.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Hi sunt filii Cham in cognationibus, et linguis, et generationibus, terrisque et gentibus suis.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 De Sem quoque nati sunt, patre omnium filiorum Heber, fratre Iapheth maiore.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Filii Sem: Aelam et Assur, et Arphaxad, et Lud, et Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Filii Aram: Us, et Hul, et Gether, et Mes.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 At vero Arphaxad genuit Sale, de quo ortus est Heber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Natique sunt Heber filii duo: nomen uni Phaleg, eo quod in diebus eius divisa sit terra: et nomen fratris eius Iectan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Qui Iectan genuit Elmodad, et Saleph, et Asarmoth, Iare,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 et Aduram, et Uzal, et Decla,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 et Ebal, et Abimael, Saba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 et Ophir, et Hevila, et Iobab. omnes isti, filii Iectan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 Et facta est habitatio eorum de Messa pergentibus usque Sephar montem orientalem.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Isti sunt filii Sem secundum cognationes et linguas, et regiones in gentibus suis.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Hae familiae Noe iuxta populos et nationes suas. Ab his divisae sunt gentes in terra post diluvium.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< Genesis 10 >