< Esdræ 2 >

1 Hi sunt autem provinciae filii, qui ascenderunt de captivitate, quam transtulerat Nabuchodonosor rex Babylonis in Babylonem, et reversi sunt in Ierusalem et Iuda, unusquisque in civitatem suam.
Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
2 Qui venerunt cum Zorobabel, Iosue, Nehemia, Saraia, Rahelaia, Mardochai, Belsan, Mesphar, Beguai, Rehum, Baana. Numerus virorum populi Israel:
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
3 Filii Pharos duo millia centum septuagintaduo.
wazao wa Paroshi 2,172
4 Filii Sephatia, trecenti septuagintaduo.
wazao wa Shefatia 372
5 Filii Area, septingenti septuagintaquinque.
wazao wa Ara 775
6 Filii Phahath Moab, filiorum Iosue: Ioab duo millia octingenti duodecim.
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
7 Filii Aelam mille ducenti quinquagintaquattuor.
wazao wa Elamu 1,254
8 Filii Zethua, nongenti quadragintaquinque.
wazao wa Zatu 945
9 Filii Zachai, septingenti sexaginta.
wazao wa Zakai 760
10 Filii Bani, sexcenti quadragintaduo.
wazao wa Bani 642
11 Filii Bebai, sexcenti vigintitres.
wazao wa Bebai 623
12 Filii Azgad, mille ducenti viginti duo.
wazao wa Azgadi 1,222
13 Filii Adonicam, sexcenti sexagintasex.
wazao wa Adonikamu 666
14 Filii Beguai, duo millia quinquagintasex.
wazao wa Bigwai 2,056
15 Filii Adin, quadringenti quinquagintaquattuor.
wazao wa Adini 454
16 Filii Ather, qui erant ex Ezechia, nonagintaocto.
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
17 Filii Besai, trecenti vigintitres.
wazao wa Besai 323
18 Filii Iora, centum duodecim.
wazao wa Yora 112
19 Filii Hasum, ducenti vigintitres.
wazao wa Hashumu 223
20 Filii Gebbar, nonagintaquinque.
wazao wa Gibari 95
21 Filii Bethlehem, centum vigintitres.
watu wa Bethlehemu 123
22 Viri Netupha, quinquagintasex.
watu wa Netofa 56
23 Viri Anathoth, centum vigintiocto.
watu wa Anathothi 128
24 Filii Azmaveth, quadraginta duo.
watu wa Azmawethi 42
25 Filii Cariathiarim, Cephira, et Beroth, septingenti quadragintatres.
wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
26 Filii Rama et Gabaa, sexcenti vigintiunus.
wazao wa Rama na Geba 621
27 Viri Machmas, centum viginti duo.
watu wa Mikmashi 122
28 Viri Bethel et Hai, ducenti vigintitres.
watu wa Betheli na Ai 223
29 Filii Nebo, quinquagintaduo.
wazao wa Nebo 52
30 Filii Megbis, centum quinquagintasex.
wazao wa Magbishi 156
31 Filii Aelam alterius, mille ducenti quinquagintaquattuor.
wazao wa Elamu ile ingine 1,254
32 Filii Harim, trecenti viginti.
wazao wa Harimu 320
33 Filii Lod Hadid, et Ono, septingenti vigintiquinque.
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725
34 Filii Iericho, trecenti quadragintaquinque.
wazao wa Yeriko 345
35 Filii Senaa, tria millia sexcenti triginta.
wazao wa Senaa 3,630
36 Sacerdotes: Filii Iadaia in domo Iosue nongenti septuaginta tres.
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
37 Filii Emmer, mille quinquagintaduo.
wazao wa Imeri 1,052
38 Filii Pheshur, mille ducenti quadraginta septem.
wazao wa Pashuri 1,247
39 Filii Harim, mille decem et septem.
wazao wa Harimu 1,017
40 Levitae: Filii Iosue et Cedmihel filiorum Odoviae septuagintaquattuor.
Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74
41 Cantores: Filii Asaph, centum vigintiocto.
Waimbaji: wazao wa Asafu 128
42 Filii Ianitorum: filii Sellum, filii Ater, filii Telmon, filii Accub, filii Hatita, filii Sobai: universi centum trigintanovem.
Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139
43 Nathinaei: filii Siha, filii Hasupha, filii Tabbaoth,
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
44 filii Ceros, filii Siaa, filii Phadon,
wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
45 filii Lebana, filii Hagaba, filii Accub,
wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
46 filii Hagab, filii Semlai, filii Hanan,
wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
47 filii Gaddel, filii Gaher, filii Raaia,
wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
48 filii Rasin, filii Necoda, filii Gazam,
wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
49 filii Aza, filii Phasea, filii Besee,
wazao wa Uza, Pasea, Besai,
50 filii Asena, filii Munim, filii Nephusim,
wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
51 filii Bacbuc, filii Hacupha, filii Harhur,
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
52 filii Besluth, filii Mahida, filii Harsa,
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
53 filii Bercos, filii Sisara, filii Thema,
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
54 filii Nasia, filii Hatipha,
wazao wa Nesia na Hatifa.
55 filii servorum Salomonis, filii Sotai, filii Sophereth, filii Pharuda,
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
56 filii Iala, filii Dercon, filii Geddel,
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
57 filii Saphatia, filii Hatil, filii Phochereth, qui erant de Asebaim, filii Ami.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
58 omnes Nathinaei, et filii servorum Salomonis, trecenti nonagintaduo.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
59 Et hi qui ascenderunt de Thelmala, Thelharsa, Cherub, et Adon, et Emer: et non potuerunt indicare domum patrum suorum et semen suum, utrum ex Israel essent.
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
60 Filii Dalaia, filii Tobia, filii Necoda, sexcenti quinquagintaduo.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652
61 Et de filiis Sacerdotum: Filii Hobia, filii Accos, filii Berzellai, qui accepit de filiabus Berzellai Galaaditis, uxorem, et vocatus est nomine eorum:
Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
62 hi quaesierunt scripturam genealogiae suae, et non invenerunt, et eiecti sunt de sacerdotio.
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
63 Et dixit Athersatha eis ut non comederent de Sancto sanctorum, donec surgeret sacerdos doctus atque perfectus.
Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
64 Omnis multitudo quasi unus, quadraginta duo millia trecenti sexaginta:
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
65 exceptis servis eorum, et ancillis, qui erant septem millia trecenti trigintaseptem: et in ipsis cantores, atque cantatrices ducenti.
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
66 Equi eorum sexcenti triginta sex, muli eorum, ducenti quadragintaquinque,
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
67 cameli eorum, quadringenti trigintaquinque, asini eorum, sex millia septingenti viginti.
ngamia 435 na punda 6,720.
68 Et de principibus patrum, cum ingrederentur templum Domini, quod est in Ierusalem, sponte obtulerunt in domum Dei ad extruendam eam in loco suo.
Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
69 Secundum vires suas dederunt impensas operis, auri solidos quadraginta millia et mille, argenti mnas quinque millia, et vestes sacerdotales centum.
Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
70 Habitaverunt ergo Sacerdotes, et Levitae, et de populo, et cantores, et ianitores, et Nathinaei in urbibus suis, universusque Israel in civitatibus suis.
Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.

< Esdræ 2 >