< Corinthios I 12 >

1 De spiritualibus autem, nolo vos ignorare fratres.
Kuhusu karama za rohoni, kaka na dada zangu sitaki mkose kufahamu.
2 Scitis autem quoniam cum Gentes essetis, ad simulachra muta prout ducebamini euntes.
Mwajua ya kuwa mlipokuwa wapagani mliongozwa kufuata sanamu zisizoongea, kwa njia zozote mliongozwa nazo.
3 Ideo notum vobis facio, quod nemo in Spiritu Dei loquens, dicit anathema Iesu. Et nemo potest dicere, Dominus Iesus, nisi in Spiritu sancto.
Kwa hiyo, nataka mfahamu kwamba hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu akisema, “Yesu amelaaniwa.” Hakuna yeyote atakayesema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa katika Roho Mtakatifu.
4 Divisiones vero gratiarum sunt, idem autem Spiritus:
Basi kuna karama tofauti tofauti, bali Roho ni yeye yule.
5 Et divisiones ministrationum sunt, idem autem Dominus:
Na kuna huduma tofauti tofauti, bali Bwana ni yeye yule.
6 Et divisiones operationum sunt, idem vero Deus, qui operatur omnia in omnibus.
Na kuna aina mbalimbali za kazi, lakini Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 Unicuique autem datur manifestatio Spiritus ad utilitatem.
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 Alii quidem per Spiritum datur sermo sapientiae: alii autem sermo scientiae secundum eundem Spiritum:
Maana mtu mmoja amepewa na Roho neno la hekima, na mwingine neno la maarifa kwa Roho yule yule.
9 alteri fides in eodem Spiritu: alii gratia sanitatum in uno Spiritu:
Kwa mwingine humpa imani kwa Roho yeye yule, na kwa mwingine karama ya uponyaji kwa Roho mmoja.
10 alii operatio virtutum, alii prophetia, alii discretio spirituum, alii genera linguarum, alii interpretatio sermonum.
Kwa mwingine matendo ya nguvu, na mwingine unabii. Na kwa mwingine uwezo wa kupambanua roho, mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingnine tafsiri za lugha.
11 Haec autem omnia operantur unus atque idem Spiritus, dividens singulis prout vult.
Lakini Roho ni yule yule atendaye kazi hizi zote, kumpa kila mtu karama kwa kadiri ya uchaguzi wake mwenyewe.
12 Sicut enim corpus unum est, et membra habet multa, omnia autem membra corporis cum sint multa, unum tamen corpus sunt: ita et Christus.
Kwa maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote ni vya mwili ule ule, vivyo hivyo na Kristo.
13 Etenim in uno Spiritu omnes nos in unum corpus baptizati sumus, sive Iudaei, sive Gentiles, sive servi, sive liberi: et omnes in uno Spiritu potati sumus.
Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wayunani, kwamba tu watumwa au huru, na wote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 Nam et corpus non est unum membrum, sed multa.
Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.
15 Si dixerit pes: Quoniam non sum manus, non sum de corpore: num ideo non est de corpore?
Ikiwa mguu utasema, “kwa kuwa mimi si mkono, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo haiufanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
16 Et si dixerit auris: Quoniam non sum oculus, non sum de corpore: num ideo est de corpore?
Na ikiwa sikio litasema, “kwa kuwa mimi si jicho, mimi si sehemu ya mwili,” hiyo hailifanyi kutokuwa sehemu ya mwili.
17 Si totum corpus oculus: ubi auditus? Si totum auditus: ubi odoratus?
Kama mwili wote utakuwa jicho, kungekuwa wapi kusikia? Kama mwili wote ukiwa sikio, kungekuwa wapi kunusa?
18 Nunc autem posuit Deus membra, unumquodque eorum in corpore sicut voluit.
Lakini Mungu aliweka kila kiungo cha mwili mahali pake kama alivyopanga mwenyewe.
19 Quod si essent omnia unum membrum, ubi corpus?
Na kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Nunc autem multa quidem membra, unum autem corpus.
Hivyo sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 Non potest autem oculus dicere manui: Opera tua non indigeo: aut iterum caput pedibus: Non estis mihi necessarii.
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “sina haja na wewe.” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, sina haja na ninyi.”
22 Sed multo magis quae videntur membra corporis infirmiora esse, necessariora sunt:
Lakini viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa na heshima kidogo vyahitajika zaidi.
23 et quae putamus ignobiliora membra esse corporis, his honorem abundantiorem circumdamus: et quae inhonesta sunt nostra, abundantiorem honestatem habent.
Na viungo vya mwili tunavyodhani vina heshima kidogo, twavipa heshima zaidi, na viungo vyetu visivyo na mvuto vina uzuri zaidi.
24 Honesta autem nostra nullius egent: sed Deus temperavit corpus, ei, cui deerat, abundantiorem tribuendo honorem,
Na sasa viungo vyetu vilivyo na mvuto havina haja ya kupewa heshima, kwa kuwa tayari vina heshima. Lakini Mungu ameviunganisha viungo vyote pamoja, na amevipa heshima zaidi vile visivyo heshimiwa.
25 ut non sit schisma in corpore, sed in idipsum pro invicem solicita sint membra.
Alifanya hivyo ili pasiwepo mgawanyiko katika mwili, bali viungo vyote vitunzane kwa upendo wa mmoja.
26 Et si quid patitur unum membrum, compatiuntur omnia membra: sive gloriatur unum membrum, congaudent omnia membra.
Na wakati kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote vyaumia kwa pamoja. Au wakati kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vyote vifurahi kwa pamoja.
27 Vos autem estis corpus Christi, et membra de membro.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
28 Et quosdam quidem posuit Deus in Ecclesia primum Apostolos, secundo Prophetas, exinde Doctores, deinde virtutes, exinde gratias curationum, opitulationes, gubernationes, genera linguarum, interpretationes sermonum.
Na Mungu ameweka katika kanisa kwanza mitume, pili manabii, tatu waalimu, kisha wale wote watendao matendo makuu, kisha karama za uponyaji, wale wasaidiao, wale wafanyao kazi ya kuongoza, na wote walio na aina mbalimbali za lugha.
29 Numquid omnes Apostoli? numquid omnes Prophetae? numquid omnes Doctores?
Je sisi sote ni mitume? Sisi sote ni manabii? Sisi sote ni waalimu? Je sisi sote tunafanya matendo ya miujiza?
30 numquid omnes virtutes? numquid omnes gratiam habent curationum? numquid omnes linguis loquuntur? numquid omnes interpretantur?
Je sisi sote tuna karama ya uponyaji? Sisi sote tunaongea kwa lugha? Sisi sote tunatafsiri lugha?
31 Aemulamini autem charismata meliora. Et adhuc excellentiorem viam vobis demonstro.
Tafuteni sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonesha njia iliyo bora zaidi.

< Corinthios I 12 >